BINADAMU HATUPO SAWA
BINADAMU HATUPO SAWA
Sura hii inaeleza kinaga ubaga kwamba
binadamu hatupo sawa hapa duniani maana yake binadamu hapa duniani ni kama vidule ambavyo havililingani ambapo
katika vidole kila kidole ni tofauti na
kidole kingine, kuna kidole kikubwa,kidogo, kidogo zaidi na hivyo kwa hali hivyo inaeleza kuwa hata binadamu wa
Duniani hatupo sawa kabisa.
Hatupo sawa kwa sababu kuna watu wenye
maisha ya chini sana na watu wenye maisha ya juu sana. Hatupo sawa kwani pia
kuna watu wazima na wenye afya zao na kuna watu wasio wazima ambao hawana afya
hata kidogo. Kuna binadamu wenye viungo vyote na kuna binadamu hawana viungo
vyote. Itoshe tu kusema kwamba duniani hatupo sawa kabisa kwani hata wewe
msomaji wa kitabu hiki haupo sawa na msomaji mwingine wa kitabu hiki.
Binadamu tumetofautiana kwa kila hali
kiuchumi, kisiasa, kijamii hata katika
maladhi, chakula, mavazi, hali hii inapelekea maisha ya dunia kuwa tofauti baina ya mtu moja
na mtu mwingine. Zipo familia ambazo haziwahi kunywa hata chain a wala hawajawahi
kupika hata chele kilo moja, na zipo familia ambazo watoto wamezoeshwa kula
wali kila iitwayo siku.
Kuna baadhi ya binadamu ambao hawafurahii
kabisa maisha ya duniani na baadhi wantamani hadi kufa maana wao hulalamika
kuwa wao ni kama wasindikizaji wa watu wanaofurahia maisha ya duniani. Huu ni
ukweli usiopingika. Mimi mwandishi wa kitabu hiki nimewahi kumuhoji mzee mmoja
ambaye aliniambia kuwa amesomeshawatoto wake wote na wtoto wake hao hawamjali
yeye kwa lolote na anapata shida kana kwamba hakuwa kusomesha. Wapo baadhi ya
binadamu ambao hawafurahii kabisa maisha
ya hapa duniani na wapo wenye fedha nyingi mno ambao hata pa kupeleka fedha
hakuna. Akisikia mtu ana shida ya fedha anaanza kushangaa, maana duniani hatupo
sawa.
Binadamu wa hapa duniani tumetofautiana
katika kila hali na hali hii ndio inaweza kuleta majivuno na unyanyasaji wa kidunia
Mtu mwenye ufahali wa kidunia anaona wenzake
hawafai, si lolote na hawana haki yoyote, lakini upande wa pili wa shilingi (Maana shilingi
ina pande mbili) tofauti zote izi
zinakuja kuondolewa na Mwenyezi Mungu ndio maana Mwenyezi Mungu amenituma
nitunge kitabu hiki kinachoitwa. KWA MUNGU WOTE NI SAWA. Kwa Mungu hakuna tofauti katika malazi, mavazi, chakula bali
binadamu machoni kwa Mungu ni sawa.lakini kwa maisha ya kifahali, kwa nyumba za
kifahari sana.
Mfano halisi tunayo, nchi za ulaya, marekani
uarabuni kuna maghorofa ambayo ni marefu sana mengine yanakaribia hadi kufika
mbinguni na yanamilikiwa na matajiri wakubwa wa duniani. Magorofa hayo yanaitwa
SKY CREEPER magorofa haya yamejengwa juu
sana lakini kwa Mungu binadamu wote ni
sawa inamaana hata Yule anayetokea kwenye nyumba za nyasi kwa Mungu yupo sawa
na hawa wanaotokea kwenye maghorofa yaliyopaa angani.
Hivyo binadamu upande wa Mungu tupo sawa
wala hakuna cheo maalumu, wala Viongozi kutengewa viti vya peke yao kama ilivyo
duniani

Maoni
Chapisha Maoni
thank you very much asante sana