DUNIANI KUNA MASKINI NA MATAJIRI
DUNIANI KUNA MASKINI NA MATAJIRI
Ni kweli kwamba hapa duniani kuna kila aina
ya masikini na matajiri wa kila aina. Kuna masikini wa kwanza na masikini wa
mwisho kwani maskini nao wanatofautiana
kutokana na madaraja walionao kama walivyo matajiri wa duniani. Kuna masikini
wa angalau na masikini ambao hawana uangalau wowote ule hata kwa kumuona tu
utaoona huyu ni maskini ambaye anahitaji msaada maana hawezi kupata chochote bila ya kusaidiwa na mtu yoyote yule.
Maskini wa kundi hili tunao katika mitaa yetu, vijiji vyetu, miji yetu, wilaya
zetu na Taifa kwa ujumla.
Pia vilevile kwa upande wa
masikini kundi hilo hilo wapo masikini
wanatokana na kukosa huduma za kijamii
kama vile chakula, maladhi ambayo ndio mahitaji ya muhimu sana kwa
binadamu
Upande wa utajiri kuna
matajiri wa kila aina vilevile pia matajiri wametofatiana kuna matajiri namba
1, namba 2 hadi namba mwisho kuna wenye uwezo mkubwa sana na wenye uwezo mdogo.
Kwa upande mwingine wa shilingi hayo makundi ambayo nimeyataja hapo juu mbele
za Mungu Muumba wetu wote ni sawa maana
yake wako ngoma droo hakuna makundi ya masikini wala makundi.
Hivyo basi Mbinguni watu wote ni sawa
haijalishi wametoka katika makundi gani lakini watu wote ni sawa haijarishi
wewe ni masikini wala wewe ni tajiri lakini watu wote ni sawa mbele ya Mwenyezi
Mungu.


Maoni
Chapisha Maoni
thank you very much asante sana