DUNIANI KUNA VYEO NA WADHIFA MBALI MBALI

 

DUNIANI KUNA VYEO NA WADHIFA MBALIMBALI

Ni ukweli usiopingika kuwa duniani kuna vyeo vya kila aina na vyeo hivyo vimetofautiana kulingana na vyeo na wadhifa wa mtu.

Upande wa vyeo kuna vyeo vya chini na vyeo vya juu na vyeo hivi vinampa mwanadamu heshima kubwa sana hapa duniani hata  anapokuwa anapita kutoka sehemu moja kwenda sehemu  nyingine au anapofanya majukumu yake binafasi vyeo hivyo vinampa heshima  kubwa sana na hali hii ndiyo inayo mtofautisha binadamu huyo na binadamu wengine.

Suala la vyeo ni jambo ambalo linajulikana dunia na vyeo hivyo vimetofautiana kuna vyeo vya juu kabisa vya heshima na vyeo vya chini. Mfano mimi binafsi ni wakili. Wakili pia  anaheshimika sana. Lakini baada ya kifo cheo nilichonacho siendi nacho mbinguni bali nitaenda na nafsi yangu mimi na  sio wakili.  Hata wewe msomaji wangu wa kitabu hiki cheo ulichonacho ni cha hapahapa  duniani ukienda mbinguni hakuna tena cheo wala wadhifa wowote ule wala hakuna saluti tena wala hakuna cha kusema simameni mheshimiwa anapita.

Mbinguni hakuna  kupigiwa makofi wala kutengewa kiti maalumu mbali mbinguni binadamu wote ni sawa.  Wadhifa wa mtu unabaki duniani baada tu ya mtu kufa na kuzikwa. Mbinguni mtu mwenye wadhifa roho yake tu ndio inayokwenda ama mbinguni au motoni kutokana na matendo aliyoyaishi.  

Itoshe kusema kinagaubaga kuwa vyeo tulivyonavyo duniani ambavyo ni vyeo vya kifahari na heshima sana ambavyo vinapatikana kutokana na kusoma, kuteuliwa au kupewa pasipo kusoma  kwa upande wa pili wa shilingi, Kwa  Mwenyezi Mungu hakuna cheo chochote kile ambacho ukifariki unaenda nacho mbinguni.

Vyeo hivi  vya duniani vinabakia hapa hapa duniani kwa hiyo tuzidi kufahamu kwamba kitabu hiki kinakufundisha  mwisho wa yote na mwisho wa vyeo vyote ni hapa hapa  duniani sababu mbinguni wote ni sawa.

 

 

 

MASKINI  NA MATAJIRI TUTUTBU DHAMBI ZETU ILI  WOTE TUMUONE MUNGU

Tunachojifunza kutokana na kitabu hiki cha Wakili JAMES LUBUS kinaeleza kwamba kwa Mungu wote ni sawa na kwa Mungu  hakuna tofauti kati ya masikini na tajiri wala cheo au wadhifa wowote ule. Bali tajiri na Masikini wote ni sawa  machoni pa Mwenyezi Mungu .

Pia kitabu hiki kinawapa  faraja sana watu wanaoishi maisha ya chini pamoja na wazee na wagonjwa kwani maisha ya duniani ni ya kupita tu lakini mwisho wa yote baada ya kufa Mungu atakupa taji lako unalostahili japo huenda ulionekana mbele ya walimwengu kama takataka machoni pa watu na haufai kabisa., au mgonjwa uliyeonekana takataka kutokana na ugonjwa ulionao na mtu ambaye hana viungo vya Mwili vyote ambaye anadhalauliwa na watu na kuonekana haufai kisa yeye ni kilema lakini kwa mwenyezi Mungu unathamani.

Kwa hiyo kwa wewe ambaye umetengwa na dunia hii kutokana na umaskini wako, ugonjwa wako uzee wako au vyovyote vile tambua kwamba kwa Mungu upo sawa kabisa na wala huna tofauti kabisa na watajiri  wa duniani.

Hivyo mwandishi wa kitabu hiki anakupa faraja kuwa ujione wewe unathamani kubwa mbele ya Mwenyezi Mungu na unastahili kupewa haki yoyote kama anazopewa binadamu ambaye hana mapungufu yoyote ya viungo.

Pia Hata kwa wewe Mzee kumbuka kwa Mungu wote ni sawa kwa hiyo kitabu hiki ni kizuri sana na kinafaa kusomwa na watu mbalimbali

Sasa nikuombe jambo moja tu ambalo Mungu atakusikiliza, nenda kwa padre kaungame dhambi zako zote na Mungu atakusamehe. Ukiungama dhambi zako zote baada ya kifo chako Mungu atakupokea vizuri sana na utasherekea vyema mbinguni.

Sasa usipoungama dhambi zako unakuwa umeishi maisha gani? Yani duniani uteseke na utengwe kulingana na umaskini wako alafu ukifa tena uende kwa shetani huko ukakutane na Moto wa milele.

 

TUKISEMA HATUNA DHAMBI TUNAJIDANGANYA”.  Ni baada ya kusoma Biblia vizuri sana kinagaubaga na kugundua kwamba kuna mistari katika Biblia inayoeleza bayana kwamba wanadamu tumejawa na dhambi, na kwamba tukisema hatuna dhambi tunajidanganya wenyewe, na kwamba binadamu tumezaliwa tukiwa na dhambi ya asili isipokuwa tu, Mama Bikira Maria mkingiwa dhambi ya asili. Madhumuni ya kuwatungia watu mbali mbali kitabu hiki  ni kuendelea kuelimisha wasomaji wa kitabu hiki kwamba sisi binadamu ni wadhambi, na hivyo ili tuweze kupata uzima wa milele, inabidi dhambi zetu tuweze kutubu. Kwa hiyo, kitabu hiki ni meli ya kukuvusha juu ya maji ili usizame bali ukamuone Mungu. Kwa tafsiri nyepsi kitabu hiki kinakusaidia wewe kumuona Mungu kwa kutubu dhambi zako. Hapo inakuwa ni kama tiketi ya moja kwa moja kutoka duniani kwenda Mbinguni.  

Pia kitabu hiki kimeeleza kinagaubaga kuwa moja ya  Sakramenti za Wakatoliki ni sakramenti ya kupata Komunio. Tunampokea Yesu kupitia umbo la mkate na divai.  Hiyo ni Imani kali ya kanisa katoliki . Yesu Kristo anakuwa yuko ndani ya moyo wako. Na Yesu Kristo ili aweze kuwa ndani ya moyo wako inatakiwa moyo wako wewe uwe na moyo ambao ni moyo msafi. Yesu Kristo hapendi nyumba ambayo siyo safi, nyumba ambayo ina wageni wengi na hapo ni pale unapo karibisha vitu vingi ndani ya moyo wako, kunakuwa na chembechembe za wizi ndani ya moyo wako.

Chembe  chembe za ushirikina, na chembe za uchawi ndani ya moyo wako. Ndani ya moyo wako kunakuwa na kiburi na dharau ya kutokumtii, mke au mume ndani ya moyo wako unakuwa na wapangaji wengi. Yesu anataka nyumba iwe haina mpangaji yoyote yule. Hivyo mwandishi wa kitabu hiki anakushauri wewe msomaji wa kitabu uondoe wapangaji wote  na baki Yesu peke yake. Njia pekee ni kufukuza wapangaji kupitia kutubu dhambi zako na unatakiwa kuungama kwa padre

BARIKIWA SANA

30.12.2025

Maoni

Machapisho Maarufu