FAIDA YA KUMSIFU MUNGU
SURA
YA TANO
FAIDA YA KUMSIFU MUNGU.
Faida
za kumsifu Mungu ni Nyingi sana kuliko hata hasara ya kutokumsifu Mungu. Tayari
unapokuwa unakuwa umeungana na waumini wengine katika kumsifu Mungu unakuwa
tayari umeanza kuonja utakatifu wa Mungu
kwa kuungana na malaika na watakatifu wote ambao wako mbinguni. Ambao na
wenyewe wanamsifu na kumtukuza Mungu . Kupitia kumsifu Mungu inakupa na wewe
haki ya kumpenda Mungu na kumsifu Mungu.
Inakupa haki ya kuonja sifa za Mungu. Inakupa haki ya kuungana na malaika na
watakatifu huko mbinguni. Maandalizi ya kujiandaa kwenda kumsifu na kumwona
Mungu kwa macho yako mwenyewe (LIVE)
Faida
za kumsifu Mungu ni kubwa sana. Maana yake HAKUJAWAHI kuwa na furaha nzuri sana duniani kama ile ya kuungana
na Mungu katika kumsifu Mungu. Hivyo ukimsifu
Mungu kwelikweli utapata faida zifuatazo
Mungu
atasikiliza maombi yako yote ya nyuma na utaona mabadiliko ya tofauti ya hali ya zamani na
hali ya sasa. Mungu atakuponya na magonjwa mbalimbali hata kama umeteseka kweli
kweli na magonjwa hayo. Mungu atakuepusha na ajali mbalimbali. Mitego ya maadui ambayo maadui
wamekutega haiwezi kukushika hata siku moja badala yake mitego hiyo itawanasa
ndugu zao. Malaika na watakatifu ambao
mtunzi wa kitabu hiki anaungana nao kupitia sifa Mungu atawatuma wakulinde vyema siku zote. Na hivyo utakuwa unakanyaga
nyayo ambazo Mungu amekanyaga hivyo hakuna wa kukuzuru. Utakuwa unakanyaga mguu
ambao amepita Mwenyezi Mungu na hivyo
unakuwa unakanyaga sehemu salama kabisa. Hata Gari ambalo wewe unaendesha au ambalo umelipanda ,
matairi yale yanakanyaga kwenye miguu ya Mungu, yani unapita barabara ambayo
Mungu ameshapita. Faida ya kumsifu Mungu ni kubwa sana kuliko
kutokumsifu kabisa. Mfano haii kupitia kitabu hiki ambacho utasoma
bure kwenye mtandao, mtunzi wa kitabu hiki pamoja na kwamba ana cheo kikubwa
sana, Wakili Msomi ameweka uwakili wake pembeni na ameamua kujishusha na kuwa
kama mkulima wa kawaida tu kwa ajili ya kumsifu Mungu. Hivyo faida za kumsifu
Mungu ni kubwa sana kwani zinakuwezesha hata wewe msomaji kupata kile
unachostahili kwa Mwenyezi Mungu. Na hivyo nasisitiza ukiwa na nafasi nzuri ya
kumsifu Mungu kwa nafasi yako, msifu Mungu kadri atakavyoona inafaa. Msifu
Mungu kadiri atakavyo kuongoza. Maana
maisha ya duniani ni mafupi sana ipo siku utahitaji kumsifu Mungu utakuwa umechelewa
kabisa. Na haya yote ili yafaanyike muombe
Mungu akupe Roho Mtakatifu. Roho Mtakatifu huyohuyo ndiye ambaye anaweza
kukuongoza kama alivyo muongoza mtunzi wa kitabu hiki kukitunga hadi wewe kukisoma na vyote hivi
amevitoa kichwani na wewe msomaji amini ninachokuambia . Siwezi kusema uongo
nitende dhambi ya bure kwa kukudanganya
mimi nakueleza ukweli kuwa sijanakili sehemu yoyote ile katika internet.
Mwongozo huu umetokana na kipaji cha Roho mtakatifu cha kutunga vitabu. Wapo
wanaosema kuwa natunga vitabu vifupi sana. Mungu alivyokupa ndio hicho kisome.
Kitabu kikiwa kikuwa sana watu wanaona uvivu kusoma . Kipaji ambacho mtunzi wa
kitabu anacho Wengi walitamani wawe kama mimi, mtunzi wa kitabu. Lakini mimi ni
nani mbele ya Mwenyezi Mungu? Mungu amenipa kipaji hiki ambacho ni kipaji adimu
sana. Hivyo basi, faida ya kumsifu Mungu ni kubwa sana na hivyo unapata baraka.
Kutoka kwake Mungu mwenyewe. Tayari umepata neema kwake Mwenyezi Mungu ambaye
ndiye pekee anayestahili kupata sifa ukimsifu Mungu pia.
Ukiwa
duniani unapata (confidence) kujiamini kwamba una kinga ya Mungu na hiyo kinga
itakukinga dhidi ya wachawi hawataweza kukugusa kabisa kamwe kama una msifu
Mungu. Unaacha alama za Mungu kinywani
mwako na hivyo kumfanya Mungu kuwepo na wewe na kuishi na wewe. Hivyo msomaji
wa kitabu hiki binafsi nakushauri uwe unamsifu Mungu kwa kuungana na malaika na
watakatifu ambao wapo mbinguni kwa ajili ya sifa na utukufu wa Mwenyezi Mungu.
Mungu akubariki sana. Barikiwa sana. Mungu akubariki sana.
LEO
CHRISMASS TAREHE 25.12.2025

Maoni
Chapisha Maoni
thank you very much asante sana