KUMSIFU MUNGU

 



 

SURA YA PILI

DOMINIKA YA  32 YA MWAKA C KUMTUKUZA MUNGU

Leo ni tarehe 09/11/2025 nimesali  Misa Takatifu Parokia ya Inyonga na Misa hiyo Takatifu  imeendeshwa na Padre mpendwa sana ambaye sitamtaja kwani sijaomba idhini yake. Masomo ya Dominica ya 32 ya maka c ndio pia yaliosababisha nikatunga kitabu hiki.  Siku ya leo ni siku ambayo ilikuwa ni siku ya kumsifu Mungu, kwani hata masomo yote ya leo yalikuwa yamelenga sifa na utukufu kwa Mwenyezi Mungu na ndio sababu kubwa iliyonichechemsha mpaka nikatunga kitabu hiki kinachoitwa

 MUNGU ANASIFIWA MUDA HUU NA  MALAIKA NA WATAKATIFU MBINGUNI

UNGANA NAO KUPITIA PAMBIO ZA SIFA NA UTUKUFU  .

 

Kilichonichechemsha mpaka nikatunga kitabu hiki ni baada pia ya kurejea kwenye kitabu changu kngine  chenye kichwa cha habari

TUMSIFU, TUMWABUDU NA TUMSUJUDIE MUNGU

Nimeelezea bayana namna ambavyo Mungu anasifiwa mbinguni. Na nimeeleza bayana kwamba Mungu aliumba mwanadamu, si kwa ajili ya kwamba mwanadamu amsifu Mungu hapana maana kabla ya Mungu kumuumba mwandamu huko mbinguni kulikuwa na viumbe wanaomsifu na kumtukuza na kumwabudu Mungu. Viumbe hao walikuwa wanatosha kabisa kumsifu na kumwabudu Mungu. Mungu alimuumba mwanadamu kwa kwa lengo  la kuungana na viumbe hao wengine waendelee kumsifu na kumtukuza Mwenyezi Mungu, ila sio kwamba alimuumba kwa ajili ya kwamba mwanadamu amsifu na kumwabudu Mungu. KAMA INGEKUWA HIVYO BASI BINADAMU WOTE WANGEENDA MBINGUNI.

 

Maneno haya yanaunga mkono kitabu changu kingine nilichotunga kinachitwa,

KUMUONA MUNGU (UTAKATIFU) NI KAZI

JINYIME YA DUNIANI UPATE TIKETI YA KUMUONA MUNGU

Hii inanesha kuwaoona viumbe wanaomsifu na kumwabudu Mungu Mbinguni ni kazi maana sio wote walioteuliwa kushuhudia Mungu akisifiwa na Malaika na Watakatifu Mbinguni ambao hutumia  vifaa mbalimbali vya kumsifu , kumtukuza Mungu , kama vile kengele, kinubi, vinanda. Na wanapiga piga vitu mbalimbali vinavyotoa sauti nzuri inayompendeza Mwenyezi Mungu huku wakiinua macho yao juu na wengine wakiwa wamelala kifudi fudi huku wakiwa wanamsifu Mungu aliye waumba na  Mungu wakiwa wamemweka katikati na huku akiwa amezungukwa na viumbe vya ajabu ambavyo vimeumbwa na Mungu mwenyewe na viumbe vingine vinachezea vinanda katika hali inayoleta furaha isiyo na kifani mbele ya kiti furani cha ajabu ambacho hakielezeki na kukiona tu unapata raha ya ajabu. Huku wengine wakiwa wanamzunguka Mungu wakifurahi tu kumuoona na wengine wakiwa wanashuhudia jinsi Mungu akiwa anasifiwa.

Wapo watakatifu ambao hawajatangazwa na Baba Mtakatifu Yeyoye Yule  nao wanashuhudua jinsi Mungu anavyosifiwa na wao wenyewe wanamifu Mungu.  Kuna kiumbe furani cha ajabu kinachezea na kupiga kinanda kwa ustadi wa hali ya juu sana na kitu furani kinapulizwa vyema hali ambayo inaleta furaha kubwa sana Mbinguni. Mungu  Muumba wa vitu vyote vinavyoonekana na visivyoonekana akiwa anaona jinsi gani anavyosifiwa. Na huku malaika watakatifu wakiwa wakishuhudia pamoja na watakatifu wengine kwa namna ambayo inaleta raha na furaha kubwa mno. Kwa upeo wangu mwenyewe mimi mwandishi nimeshindwa namna ya kuelezea ila kama umenielewa ni furaha isiyo na kifani   na haifananishi na sherehe, tafrija, mkesha wowote ule  hata sherehe zisizo na kifani za ulaya au bara loote lile hazifiki hata chembe ya mchanga mdogo.

Hii ni kwa namna ambayo sitaweza kuielezea ambavyo ipo, lakini ni namna ambayo inaleta shangwe kubwa sana kuliko shangwe yoyote ile ambayo ipo duniani au kokote kule duniani au kwenye sayari yoyote ile.

Hii ni shangwe na sherehe na tafrija kubwa sana ndio maana hata katika bibilia imeeleza bayana kuwa siku  moja mbinguni ni sawa na miaka elfu moja . Soma 2 petro 3.8.

 Mungu ndiye wa ajabu na mwenye utakatifu mkubwa sana kuliko kiumbe chochote duniani kuwahi kutokea. Ndio maana kama nilivyoeleza hapo awali kwamba  kwa Mungu miaka elfu moja ya duniani ndio sawa na  siku moja iliyoisha tu yani ya jana. Nimejifikirisha na nimemuona Mwenyezi Mungu kwa namna ambavyo malaika hao wanamsifu Mungu akiwaona, lakini Mungu sijamwona maana ukimuuona Mungu basi unakufa.

MUNGU ni Roho,” na wanadamu hawawezi kumwona. Hayo ni kutokana na maandiko katika Yohana 4.24. Hata hivyo, Biblia inataja watu ambao walimwona Mungu kwa njia Fulani. Soma Waebrania 11.27

Linganisha hali yetu na ya mtu aliyezaliwa kipofu. Je, upofu wake unamzuia kabisa kuelewa mambo yanayomzunguka? La hasha. Mtu aliye kipofu hupata habari kupitia njia mbalimbali zinazomwezesha kutambua watu, vitu, na shughuli zilizo karibu naye. Mwanamume mmoja kipofu alisema hivi: “Mtu haoni tu kwa macho. Akili inahusika pia.” Ndio maana mtu aliyezaliwa hana macho huenda shule, na ana haki ya kuwa na familia kama wengine.

Vivyo hivyo, ingawa huwezi kumwona Mungu kwa macho halisi, unaweza kutumia “macho ya moyo” wako kumwona. Mimi mwandishi wa kitabu hiki, pale pia ambapo ninapomuomba Mungu anikinge na anilinde na maadui zangu hasa hasa wa njia ya kelekea Tabora, huwa nafumba macho na kuvuta taswira kwa ukaribu huku nikivuta imani kubwa kuwa Mungu ananioona na ananipigania na adu hao. Ndio maana kila wakiweka mitego hainasi , kumbe mitege hiyo wanajiwekea wenyewe kupia  Mungu mwenyewe.

 Hata katika kitabu changu kingine chenye kichwa cha habari

MUMGU YUPO KWELI, MAAJABU YA MUNGU KATIKA UUMBAJI WA DUNIA, niijaribu kuweka picha ya Mungu niliikosa kwenye mtandao bali niliweka picha ya maajabu  tu ya Mwenyezi Mungu.

Mungu haonekani wala hajulikani yupoje. Ni fikra tu ya kufikiri namna ambavyo Mungu yupo. Kwa hiyo kitabu hiki kitakufaa sana. Uwe mtoto mdogo sana, wewe kaka, shangazi, Mjomba. Wewe mtu wa Mungu. Kiongozi mkuu wa dini. Mwanajumuiya wa mwenyekiti wa jumuia mbalimbali vigango.

Kupitia kitabu  hiki utapata baraka na neema sana ambazo zitaongezeka moja kwa moja pia  mtunzi wa kitabu hiki naye  atapata baraka na neema kutokana na wewe kusoma kitabu hiki ambacho ametunga mwenyewe na wala hajakopea sehemu yoyote ile.

Kadri unavyoendelea kusoma kitabu hiki pia na mtoto wako , naye atapata baraka na neema kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

Kitabu hiki ambacho kipo tofauti kabisa  hakijawahi kuandikwa na mtu yeyote yule hapa duniani. Kama wewe ni mtaalamu wa Komputa jaribu kuingiza maneno haya kwenye komputa uone kama yana fanana na mwandishi yoyote yule. Jibu ni hapana. Maandishi haya yatadumu kuliko hata umri wa mwandishi au msomaji na mwisho wa kiama  nitakuja niletewe kitabu hiki mbinguni. Kwahiyo tuendelee kumwabudu na kumsifu Mungu pekee.

Najuwa wapo watu wenye kudharau hili ambao wao kutwa nzima wanashinda kwenye mitandao kuangalia picha za utupu na picha ambazo hazimpendezi Mungu badala ya kufuatilia na kusambaza neno la Mungu kadiri ambavyo Mungu mwenyewe ameingia rohoni mwa mandishi wa kitabu hiki mpaka akatunga kitabu ambacho sasa wewe mtumishi wa Mungu uliyeteuliwa unakisoma. Maana asiye mtumishi wa Mungu kazi yake itakuwa ni kutoa kejeri, dharau, kukashifu kitabu hiki cha Mungu badala yake yupo tayari kutoa maoni kwenye picha za wadada ambao wamevaa nusu Uchu, wadada wadangaji ambao viuongo vya miili vinaonekana kwa macho kinyume na taratibu. Hapo kupata Baraka  itakuwa ni ndoto.

Hata napo napenda kuelezea jambo. Kwani kuna ubaya gani mtu akiwa ni wakili kutumiwa na Mwenyezi Mungu kufikisha neno la Mungu?

Ukitaka kuona kuwa kitabu hiki ni cha ajabu, kama ndugu yako anaumwa kichape kitabu hiki alafu nyuma ya kitabu hiki andika maneno haya

MUNGU MPONYE MGONJWA  WANGU KISHA ANDIKA NA MAOMBI YAKO ALAFU  CHOMA UKURASA ULIOONDIKA MAOMBI  subiri sasa mgonjwa wako apone.

Imani ndio kila kitu

BARIKIWA SANA

Maoni

Machapisho Maarufu