MALAIKA NA WATAKATIFU WANAMSIFU MUNGU MBINGUNI

 


SURA YA NNE

MALAIKA NA WATAKATIFU WANAMSIFU MUNGU MBINGUNI.

Sura ya tatu nimeeleza bayana vifaa ambavyo vinatumika kumsifu Mungu ambavyo hakuna haja ya kuvitaja tena. Inaeleza bayana vifaa hivyo vinatumiwa na malaika, watakatifu wengine akiwepo pamoja na Padri Luka.

Biblia imeeleza bayana katika mistari mingi mingi sana ambayo itachukua muda sana kuelezea namna ambavyo watakatifu, Malaika na wenye heri wanavyo msifu Mungu mbinguni. Watakatifu hao wamegawanyika katika makundi mbalimbali. Kuna wanaomsifu Mungu na kumsujudia Mungu. Kuna ambao wamelala  kifudifudi. Wote lengo lao ni moja la  kumsifu Mungu na kumwaga sifa kemkem  kwake.  Viumbe vyote vinavyoonekana na visivyoonekana vyote vinaamini   kwamba anayestahili kupewa sifa ni Mwenyezi Mungu tu. Muda huu unaposoma kitabu changu sifa zote zinamwendea Mwenyezi Mungu na  Mwenyezi Mungu  akazipokea sifa hizo.  Muda huu unaposoma kitabu Fumba macho kwa imani kubwa ungana na malaika na watakatifu wanaomsifu Mungu muda huu kama jina la kitabu linavyosema kuwa MUMGU ANASIFIWA NA MALAIKA NA WATAKATIFU MBINGUNI UNGANA NAO KUPITIA PAMBIO

Kwa imani tunaamini malaika na watakatifu baadhi wakiwa mbele  wengine wakiwa juu, wengine wako pembeni kulia na kushoto wakiwa wanamwabudu Mungu na kumsifu Mungu.

Pia Padre Pio ambaye pia nimetunga kitabu cha kwake ambacho kimeeleza kwamba Padre Pio utuombee pamoja na padre Walter Luekewille ambaye naye nimeeleza kwa maisha aliyoishi duniani ameacha alama za kikiristo miyoyoni mwetu.

Ungana na badhi ya Watakatifu waliotangazwa  na hata wale wasiotangazwa ambao wamebeba majina ya jumuia zetu, vigango vyetu na majina ya parokia zetu.

Somo wangu James, wapo malaika, walinzi wa aina mbalimbali wapo viumbe wasioonekana ambao sisi binadamu hatujui wakoje. Wote wapo kwenye mstari mmoja wa kumsifu Mungu huku wakitoa sauti nzuri sana. Sauti zenye harufu njema na maua safi ya kumsifu Mungu na huku wakiimba wakisema, Hosana juu mbinguni.

Sifa na utukufu kwa Mwenyezi Mungu ambaye aliumba viumbe vyote vinavyo msifu Mungu vimetoka kwake Yeye Mwenyezi Mungu pamoja na mtunzi wa kitabu hiki ambaye anatumia kitabu hiki kumsifu Mungu. Na yeye mtunzi wa kitabu hiki naye ametoka kwa Mwenyezi Mungu, na kwake Mwenyezi Mungu atakuja kurejea na kumsifu milele na milele.

Kupitia kitabu hiki anaamini kitapokelewa baada ya wasomaji kukisoma bure kabisa kwenye mtandao.

Kupitia kitabu chake kingine  chenye kichwa habari  ‘Mungu ndiye tajiri wa matajiri’ naomba umuombe Mungu akupe tone ya utajiri kidogo tu kama incha tu ya ukucha wako.

Namuomba Mungu pia aniwezeshe siku moja mimi mwandishiwa kitabu hiki nije nipate fedha niende nikalione kaburi la Hayati padri Luka, pamoja na makaburi ya baadhi ya Watakatifu huko Ulaya.

Hivyo wewe msomaji wa kitabu hiki ungana pamoja na mtunzi wa kitabu hiki katika kumsifu Mungu pamoja na malaika Mbingun. Sisi Wakatoliki ambapo muda wa kuimba ukifika tunaimba na kumsifu Mungu, kwani hakika sifa zote zinatakiwa sifa zote zimwendee Mwenyezi Mungu.  Hatuwezi kumlipa Mwenyezi Mungu  kwa mengi anayotufanyia zaidi zaidi ya kuungana na watakatifu wote wa mbinguni na duniani katika kumsifu Mungu. Kupitia vifaa ambavyo nimeeleza katika sura iliyopita.

 

 

 

 

Maoni

Machapisho Maarufu