MUNGU ANASIFIWA KWA VINUBI, VINANDA, ZEZE, KENGELE VINGWENGWE NA VIFAA VINGINE

 

SURA YA TATU


MUNGU ANASIFIWA KWA VINUBI, VINANDA, ZEZE, KENGELE VINGWENGWE NA VIFAA VINGINE

Katika hali ya kumsifu Mungu, vifaa hivi vinatumika na binadamu katika hali ya kumsifu na kumwabudu Mungu. Vifaa hivi ni kama vile gitaa, vinanda, filimbi, tarumbeta, ngoma, zeze, marimba, vinubi, vigenge, kengele. Ni vifaa vinavyotumika na  mwanadamu wa hapa duniani katika kumsifu Mungu.Huku baadhi wakiwa wanapiga makofi ili  kusifia Mungu katika Roho ya kweli.

Vifaa hivi hivi ambavyo vimetengenezwa na binadamu hapa duniani vikitumika vizuri sauti yake huweza kupenya moja kwa moja na kumfikia Mwenyezi Mungu kwa imani kubwa Mungu hupokea sifa hizo na anayetoa sifa hizo Mungu humpa fungu lake na wala hawezi kamwe kumsahau na mwisho wa maisha yake ya hapa duniani, Mungu huyo huyo anaweza akamwita kwake ili aweze sasa kumuoona kwa macho yenyewe(Waswahili husema amuone LAIVE) endapo pia ataacha dhambi zake na kutubu dhambi zake na kuishi maisha ya utakatifu.

Tunafahamu kabisa kwamba vifaa hivi vinatoa sauti nzuri yenye kutoa hamasa zenye kuleta raha, kumfanya mtu ajisikie vizuri hivyo vifaa vinatumika mbinguni kumsifu Mungu. Vifaa vya muziki vipo vingi sana na vyote vimetengenezwa na mwanadamu ambavyo pia vinaweza kutumika kumsifu Mungu pekee.

Vifaa ivi ivi pia huweza pia kumchangamsha mwanadamu wa hapa duniani pale anapokuwa hana furaha  na hivyo kumpa faraja na vinamfanya aburudike. Vifaa hivi vikitumika kwa lengo la kumsifu Mungu, hupokea sifa zake kwa baadhi ya binadamu wanaojua kusifu na kumwabudu Mungu .Kwa sisi Wakatoliki huwa kabla ya kuanza kusifu huwa tuna omba toba kupia wimbo wa  EE bwana utuhurumie. Baada ya wimbo wa bwana utuhurumie kuna wimbo wa utukufu kwa MUNGU

Hapo wakati wa azimio ya Misa Takatifu sisi wakatoliki tunaungana na wakatoliki wengine duniani kote katika kumsifu Mungu kupitia wimbo huo wa Utukufu kwa Mungu Mwenyezi

Katika wimbo huo vifaa nilivyovisema hapo juu ambavyo ni vinanda, filimbi, tarumbeta, ngoma, zeze, marimba, vinubi, vinanda, vigenge hutumika kutoa sifa kwa Mwenyezi Mungu. Mbele ya wana kwaya watoto waliovaa sare hucheza  cheza kwa step nzuri yenye madowido wakiwa wanaimba wimbo wa utukufu kwa Mwenyezi Mungu. Wimbo huu ambao unatumika pia kumsifu Mwenyezi Mungu kwa yote ambayo Mungu ameyaumba au kuyafanya hapa duniani. Vifaa vingine kama ivi  vinatumika kumsifu Mungu mbinguni. Hivyo malaika na watakatifu humsifu Mungu kupitia mpigaji maalum wa vifaa hivyo  ambaye hupiga kwa madhumuni ya kumsifu na kumtukuza Mungu kuwa pia kuna viumbe wasioonekana nao humsifu Mungu kwa namna yake viumbe hao wakiwa  kifudifudi huku viumbe hao wakimsifu Mungu kwa kumpigia kelelza shangwe  Kelele hizo za sifa huwa zipo katika mchujo wa sauti nzuri, nyororo yenye kuvutia, zenye kutia hamasa ambayo Mungu hupendeza kuzisikia tu. Viumbe hao wasionekana huungana pia na  Watakatifu na malaika wa mbinguni ambao humsifu Mungu na kumtukuza kupitia vifaa hivi vya kumsifu na kumwabudu Mwenyezi Mungu. Na hivyo kufanya zoezi zima la kumsifu Mwenyezi Mungu lilete maana nzuri ya kumsifu na kumwabudu Mungu.

Viumbe hao wasioonekana pia watafikisha kitabu hiki cha kumsifu Mungu ili pia Mungu aweze kuyakubali maombi kumi ya mwandishi aliyoomba na kutia nia na hatimaye kuyachoma juu ya Mlima Itwele.

Zoezi hili la kumsifu Mungu kwa kuungana pamoja na Watakatifu na Malaika wa Mbinguni hata wewe mwanadamu ambaye upo duniani unaweza ukatumia muda wako mzuri wakati wa uhai wako kumsifu Mungu na kuungana na malaika na watakatifu kupitia zeze na vinanda . Mungu anasikia sauti nzuri inayompendeza YEYE Hatimaye, baada ya kumsifu Mungu sasa unaweza ukaomba lolote lile na Mungu kupitia Mungu mwenyewe atapokea maombi yake yote, na Mungu atakusamehe dhambi zako zote na mwisho wa siku utafika katika ufalme wake. Pia  sifa za kumsifu Mungu zitakusaidia kupata mema yote yanayostahili duniani

Maoni

Machapisho Maarufu