MUNGU HUZIOONA DHAHABU KWA MACHO YAKE

 


SURA YA NNE

MUNGU ANAJUWA DHAHABU ZIPO WAPI

Ni ukweli ambao haupingiki na ukweli wowote kuwa kwa Mwenyezi MUNGU ndiye aliyeumba madini yote yanayoonekana na yasio onekana pia anajuwa madini haya yapo wapi. MUNGU huyatazama madini moja kwa moja tofauti na sisi binadamu ambao tunatumia vifaa mbali mbali kuyatafuta baadhi ya Madini ambayo pia huenda tusiweze kuyapata au kuyaoona.

Hayo ni moja ya maajubu ya Mwenyezi MUNGU.

Ni sawa na wewe msomaji wa Kitabu hiki kama una mali umeizificha mahali lazima ujue kwamba mali hizo umezificha au umeziweka wapi  na wala huhitaji usaidizi wa  namna  yoyote ile kwani mali hizo unakuwa unajuwa umezihifadhi wapi.

 

Huo ndio ukweli usiopingika kwamba katika dunia hii kuna mali nyingi sana ambazo ni MUNGU pekee anajuwa mali hizo za gharama zipo wapi. Mwandishi wa kitabu hiki ameoteshwa kwamba ndani ya Tanzania kuna mawe ya dhahabu ambayo yameshikana yenye matani kwa matani ambayo yakibahatika kuonwa basi Tanzania inaweza kuwa ya kwanza kwa utajiri. Ila Muda haujafika wa kuweza kufahamu huo mwamba wenye madini yenye thamani.

Na ndio maana machimboni huwa kuna kuwa na waganga wa kienyeji ambao huwa wana angua kuwa sehemu furani kuna madini wana mchanja dawa huyo mtu anaenda kuchimba. Ila kwa kuwa mwandishi wa kitabu hiki haamini waganga hao anaamini kuwa huo ni Wizi kama wizi wingine kwani kama mganga anajuwa hayo madini yapo wapi si aende mwenyewe akachimbe.

Hivyo ninao uthubutu wa kumsifia Mungu kuwa yeye ndiye tajiri wa matajiri wote duniani hapa na huko kwingine .

Mfano halisi tunao, hata uwe mwema kiasi gani huwezi kumpa jirani zako mali zako zote. Mfano huo ndio mfano hai. MUNGU hawezi kumpa binadamu utajiri wote wa hii dunia maana ni ukweli usiopingika kuwa MUNGUanaogopa kumpa binadamu utajiri wote kwani ndio atakuwa anampoteza huyo mtu badala ya kumpata.

 

 

 

Maoni

Machapisho Maarufu