MUNGU NDIYE TAJIRI WA MATAJIRI

 


SURA YA TANO

MUOMBE MUNGU AKUPE SEHEMU YA UTAJIRI

Ni ukweli usiopingika kuwa vitu vyote ni vya Mwenyezi MUNGU na kwake mbinguni tutarejea na kuviacha, ila msomaji wa kitabu hiki Muombe MUNGU aweze kukupa hata  chembe ndogo tu ya utajiri wa mwenyezi MUNGU ili na wewe uishi kama binadamu wengine. Ukifuatilia pia vizuri sio kila kitu unachomuomba mwenyezi MUNGU anakupatia kwa wakati. La hasha. Kuna wakati muda wa kupatiwa unachomba unakuwa haujafika na nakuomba usikate tamaa maana Mungu hajibu siku moja.

Kuna wakati MUNGU hampatii binadamu kile anachoomba kwa sababu anajuwa pia akimpatia ndio itakuwa mwanzo mwisho wa huyo  binadamu kumtumikia MUNGU maana ataanza kuabudu na kutumikia mali ambazo MUNGU amempatia.

Kuna baadhi ya wasomaji watapenda sura hii ya tano huku wakiamini kuwa ni kupitia maombi tu MUNGU atawapa utajiri. Jibu ni sio kweli. Ninavyosema omba MUNGU akupatie sehemu ya utajiri ni pamoja na wewe kujibidisha katika shuguri zako za kila siku kama vile ufugaji, kuuza mchele, biashara ya genge, kuwekeza katika kilimo na kufanya shuguri mbali mbali. Sio kushinda na bibilia ukiketi kuomba toka asubuhi hadi jioni ukisubiria miujiza ya Mwenyezi MUNGU.

Mwandishi wa kitabu hiki anvyosema Muombe MUNGU akupe sehemu ya utajiri anakutaka pia ufanye kazi na uwe mbunifu alafu MUNGU sasa akutangule kwenye kazi zako za kila siku hapo utatoka kwenye hatua moja na utaenda kwenye hatua nyingine.

Kikubwa pia n kumuomba MUNGU akupe afya njema na afya hiyo ndio itakuwezesha wewe kupata utajiri

Basi msomajiwa kitabu changu muombe MUNGU akupe hata kiasi kidogo cha mali au utajiriwa ahapa duniani



Maoni

Machapisho Maarufu