MUNGU NDIYE TAJIRI WA MATAJIRI

 


ü SURA YA KWANZA

ü MUNGU NI TAJIRI WA MATAJIRI

ü Kilichonishawishi mpaka kupata kichwa cha habari hiki ambacho ni kichwa cha habari adimu  duniani kote hakijawahi kutungwa hapa Tanzania na mtu yeyote Yule, ni kwa  uwezo wa Mwenyezii MUNGU ambaye alinitokea kupitia ndoto na kupata maono kwamba natakiwa nitunge kitabu hiki na kukiposti kwenye mitandao mara moja nisipofanya hivyo nitakufa ili mataifa waweze kujua na kukiri kuwa MUNGU ndiye Tajiri wa Matajiri, na hii pia ni njia mojawapo ya kumsifu, na kumtukuza MUNGU.

ü Nimetunga vitabu vitano vya kumsifu sana MUNGU, vitabu hivyo sijakopea au kunakiri sehemu yeyote ile bali ni kipaji kutoka kwake. Huenda MUNGU mwenyewe alitaka kufikisha ujumbe kwako wewe msomaji kupitia Wakili   James Lubus. Mimi ni nani mbele ya MUNGU mpaka niandike vitabu mbali mbali mia moja. Maana wengi walitamani wawe kama mwaandishi wa vitabu kama mimi wakili. Ila MUNGU ametoa vipaji kila mtu na kipaji chake. Kuna mengine ambayo hata mimi mwandishi wa kitabu siwezi kuyafanya ila unakuta anayayafanya mtu asiyejuwa hata kusoma.

ü Moja ya vitabu vya kumsifu MUNGU ni

ü MUNGU ANASIFIWA NA MALAIKA NA WATAKATIFU WOTE MBINGUNI,  UNGAMA NAO KUPITIA SALA NA PAMBIO

ü MBINGUNI  RAHA, KUSIFU NA KUABUDU KILA SIKU

ü KUMUONA MUNGU(UTAKATIFU) NI KAZI

ü TUMWABUDU NA TUMSIFU NA TUMSUJUDIE MUNGU

ü KWA MUNGU WOTE NI SAWA

ü NATAMANI KUISHI BAADA YA KUFA

ü MUNGU TAJIRI WA MATAJIRI

ü NAMPENDA MUNGU NITAUNGAMA DHAMBI ZANGU NIPATE UZIMA WA MBINGUNI

ü MAAJABU YA MUNGU KATIKA UUMBAJI WA DUNIA

ü MUNGU YUPO KWELI

ü N.K

ü Namshukuru MUNGU kwa kupata upendeleo maalumu wa kuniwezesha  mimi kutunga kitabu kipya kinacho sema MUNGU NDIYE TAJIRI WA MATAJIRI

ü Ujumbe wa Mwenyezii MUNGU kupitia kipaji cha Wakili JAMES  LUBUS, ni baada  ya kuona matajiri wengi wa dunia jinsi ambavyo wanashindwa kumshukuru MUNGU kwa huruma yake, ambaye ameweza kuwapa Utajiri wa kipekee mpaka wakangia kwenye Record ya Matajiri Tanzania, Africa Mashariki na  Africa hatimaye Duniani

ü Pasipokujuwa kwamba kila kinachoonekana Duniani kimeumbwa na Mwenyezi MUNGU pekee. Sisi binadamu hata tuwe na uwezo gani huwezi ukaunda hata ka mchicha. Kwenye kitabu changu kinachoitwa, MUNGU YUPO KWELI, nimeeleza ukweli kwamba kila unachokiona kimeumbwa na Mwenyezii MUNGU. Ila binadamu hawezi kutengeneza hata kiumbe chochote kile akakipa uhai.Tumesikia Simulizi mbali mbali kuwa huko Ulaya Wazungu walitengeneza Mwanadamu anayeongea ukimuuliza swali anajibu,  hana punzi ya Mwenyezii MUNGU.

ü Ukifuatilia masimulizi mbali mbali kuna ROBOT moja anaitwa SOPHIA , Robort hiyo huongea na kujibu maswali lakini sio binadamu. Hapa duniani kila kitu unachokioona kimeumbwa na Mwenyezii MUNGU na hii inamaana  kuwa MWENYEZII MUNGU NDIYE TAJIRI WA MATAJIRI NA NDIYE muanzilishi  na muasisi wa vitu vyote unavyoviiona na visivyoonekana. Ina maana kwa sisi Wakiristo WAKATOLIKI KUPITIA SALA ya Nasadiki kwa vitu vyote vinavyoonekana na visivyoonekana.

ü Bado tunaamini uwa kuna viumbe vya ajabu sana ambavyo havionekani kabisa lakini vimeumbwa na mwenyezi MUNGU.

ü Ndio maana kuna viumbe vingine kuvioona mpaka utumie darubini kali.

ü Hivyo  ukiona tajiri anajidai na mali zake  anakuwa hajitambui tu kuwa hizo ni mali za Mwenyezi MUNGU yeye ameazimwa tu kwa Muda. Hata mwandishi wa kitabu hiki anamiliki gari nne lakini zote hizo sio mali zake richa ya kwamba kwenye kadi ya gari yameandikwa majina yake.

ü Pia mwandishi wa kitabu hiki anamiliki mali nyingi tu ila hawezi kujivuna kwani vyote ni mali za mwenyezi MUNGU.

ü Tofauti sasa na mwandishi wa kitabu hiki, kuna baadhi ya watu wanamilki mali kidogo tu ila kila siku zinawaleta majivuno na wanajivubia kweli kweli kwamba wao wapo tofauti na wengine. MUNGU hapendi kabisa.

ü na vitu alivyopewa na  kuna vitu ambavyo wengine wamenyimwa inamaana anajidai kwa maana vitu hivyo vimetoka kwa MUNGU kwa maana yeye ndiye anayeumba vinavyoonekana na visivyoonekana

Maoni

Machapisho Maarufu