OROZA YA MATAJIEI TANZANIA

 


SURA YA PILI

Orodha ya Matajiri Tanzania

Sura ya pili italeta maana nzuri ya kumuelezea MUNGU kuwa ndio tajiri wa matajiri duniani ina maana hata hawa matajiri mali zao zote wamepewa na yeye Mwenyezi MUNGU , orodha ya matajiri ni kama ifutavyo.

 

1. Mohammed Dewji (Mo Dewji) – Dola Bilioni 1.8

Bilionea huyu kijana ni Mkurugenzi Mtendaji wa MeTL Group, kampuni inayofanya shughuli zake katika zaidi ya nchi 10 barani Afrika. Mo amewekeza katika uzalishaji wa bidhaa kama mafuta ya kupikia, vinywaji, sabuni, nguo na hata usafirishaji. Mbali na biashara, Mo pia ni miongoni mwa wafanyabiashara wachache walioahidi kutoa sehemu ya utajiri wao kusaidia jamii kupitia mpango wa Giving Pledge.

2. Rostam Azizi – Dola Bilioni 1.04

Rostam si tu mfanyabiashara bali pia ni mwekezaji mwenye uzoefu mkubwa katika sekta ya mawasiliano, gesi asilia, na mali isiyohamishika. Aliwahi kuwa mbunge na amekuwa na ushawishi mkubwa katika siasa na biashara nchini.

3. Said Salim Bakhresa – Dola Milioni 900

Ikiwa umewahi kutumia bidhaa za Azam, basi tayari unaujua mchango wa Bakhresa Group kwenye maisha ya kila Mtanzania. Kuanzia kwenye chakula, usafirishaji wa baharini, hadi runinga ya Azam TV, Bakhresa ameweka alama kubwa kwenye uchumi wa Tanzania.

4. Ally Awadh – Dola Milioni 600

Awadh amejijengea jina kubwa kupitia biashara ya mafuta na vituo vya mafuta vilivyoenea nchini kote. Ujasiriamali wake umemfanya kuwa miongoni mwa vijana waliofanikiwa kwa kasi katika miaka ya karibuni.

5. Shekhar Kanabar – Dola Milioni 390

Anajulikana kwa biashara ya vifaa vya magari – hasa betri, tairi na vipuri. Ni mfano mzuri wa jinsi sekta ya vipuri vya magari inaweza kugeuka kuwa fursa kubwa ya kifedha kwa wenye maono.

6. Fida Hussein Rashid – Dola Milioni 145

Fida amejikita zaidi kwenye biashara ya magari na ujenzi wa majengo ya kifahari. Anaonekana kuwa mwekezaji mahiri katika sekta ya mali isiyohamishika.

7. Yusuf Manji – Dola Milioni 20.4

Japo amekuwa kimya kwa muda, Manji aliwahi kutikisa jiji la Dar es Salaam kupitia uwekezaji kwenye viwanda, ujenzi, na hata michezo. Ana historia ya kuwa mmoja wa watu waliowahi kuwekeza fedha nyingi katika klabu za soka Tanzania.

8. Ghaleb Said Mohammed – Dola Milioni 15.3

Mfanyabiashara huyu amewekeza katika huduma za kifedha, majengo ya kibiashara, na vyombo vya habari. Anaendelea kupanua shughuli zake ndani na nje ya nchi.

9. Yogesh Manek – Dola Milioni 9

Amejikita katika benki, bima na huduma za afya. Manek ameonyesha kuwa sekta ya fedha ina nafasi kubwa katika kujenga utajiri wa muda mrefu.

10. Abdulaziz Abood – Dola Milioni 8.5

Mbunge wa zamani na mfanyabiashara mashuhuri anayehusishwa na biashara za usafirishaji, mafuta na vyombo vya habari.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Maoni

Machapisho Maarufu