SURA YA TATU

UTAJIRI KATIKA MAHITAJI MAKUU YA BINADAMU

 

Hivyo basi mahitaji makuu muhimu ya mwanadamu yapo matatu ambayo ni chakula,malazi na mavazi.Ili ujitoshereze kuwa tajiri inatakiwa umudu haya mahitaji yote na uyapate kwa upendeleo mkubwa sana . Hii ina maana kwamba wakati baadhi ya binadamu wengine wanahangaika na kuwaza kwa undani wapi watapata mahitaji haya matatu, wewe uliyejaliwa na MUNGU mpaka unaanza kukufuru kwamba hee kumbe kuna watu wana shida vyingi Duniani.

 Tukianza  na chakula ni ukweli usiopingika  kuwa matajiri ndio wanaongoza kula chakula chochote wanachokitaka  bali maskini anakula chakula chochote kile kinachopatikana au kinachokuwa mbele yake na haijalishi chakula hicho ni kizuri au sio kizuri. Maskini anakula bora chakula na tajiri anakula chakula bora na kitamu.   Kuna baadhi ya matajiri wana uwezo wa kula chakula wanachokitaka au kukihitaji hata kama chakula hicho kinaweza kikawa kipo bara lingine yupo tayari kuingia gharama kukifuata hicho chakula ili aweze kukipata.  Hivyo yupo tayari kwenda Ulaya kula chakula cha mchana tu kwa kuruka na ndege. Maajabu ya mwenyezi MUNGU yapo hapa kwa matajiri. Kuna baadhi wana fedha ya kununua kila kitu ila MUNGU naye  akawanyima hamu ya kula  ambayo huwezi kuipata dukani maana hamu ya kula huwezi kinunua duka la lolote lile la madawa. Hata wale wanaouza vidonge vya kuongeza hamu ya kula yani Vitamai C  haifanyi kazi kama  hamu ya kula ya asili ya Mwenyezi MUNGU, maana yake hamu ya kula chakula inayoitwa ‘’ apetaiti’’ hata kama ukiwa na fedha  namna gani huwezi kununua apetaiti ya kula chakula.

Upande wa malazi, malazi yanayozungumziwa hapa si malazi ya magonjwa inamaana sehemu ya kujisitiri kama nyumba za magorofa makubwa hata nyumba za kawaida hata ya nyasi pia ni malazi MUNGU mwenyewe ndiye anawezesha binadamu kuwa na malazi kwa kiwango tofauti ipo kama vile vidole ambavyo haviwezi kulingana utaifa  au rangi kama watu wenye rangi nyeupe walivyojaliwa  kuwa na malazi mazuri kama marekani, uarabuni nk, na sio Afrika kipekee nipende kumshukuru MUNGU kwa kuandika kitabu hiki watu wapate kujua kuwa MUNGU ndiye tajiri wa matajiri duniani.

Ipo ivi maladhi ndio yanayomuonesha mtu au yanayotambulisha utajiri wa mtu mmoja na mtu mwingine. Mtu anayetoka kwenye nyumba ya nyasi na anayetoka kwenye nyumba ya bati lazima watu hawa wawe tofauti kabisa.

Wengi wanatamani kweli kuwa na makazi bora ila sasa vifaa vimepanda bei balaa na nyumba ukiipauliwa inaanza sasa kuongea kiingereza inahitaji, tiles, skimming, bandaring, na malembo mazuri ya kisasa. Nenda ukaulize bei ya vitu hivyo dukani ni fedha nyingi sana.

Hakuna mtu anayetaka kuishi maisha ya dhiki na shida ni hali tu ndio haziruhusu kabisa kama nilivyosema awali kuwa binadamu si sawa na vidole havilingani.

Na hali hiyo ndio inayomtoafutisha maskini na tajiri japo hata maskini wenyewe nao wapo kwenye madaraja. Kuna maskini mwenye unafauu kuliko wengine na kuna maskini ambaye hata ukimuona utasema huyu ni Maskini. Kuna maskini ambaye hana viuongo vyote na kuna maskini ambaye ana viungo vyote ila amekosa tu mahitaji ya kibinadamu.

Vile vile hata matajiri nao wametofautiana tajiri kwa matajiri. Kuna matajiri ambao wapo daraja la kwanza yani hao ndio ambao wapo kwenye orodha ya matajiri na kuna matajiri ni matajiri kwa kupata mahitaji tu ya masingi ila  hawapo kwenye orodha ya matajiri.

Vilevile watu wenye malazi makubwa ndio wanajulikana kama matajiri na watu wenye malazi madogo ndio wanatambulika kama masikini wakubwa duniani. Hivyo MUNGU ndiye anayeweza kuumba vinavyoonekana na visivyoonekana hata chini ya ardhi MUNGU anajua yaliyomo hata baadhi ya madini chini ya ardhi mfano kwa Tanzania ukipata madini unakuwa tajiri wa dunia nzima. MUNGU anaweza kukupa uwezo wa kumiliki madini na wapi  kwa kupata madini hili liwe fundisho kwa matajiri wote duniani pamoja na kuwepo kwa matajiri wote duniani MUNGU ndiye tajiri namba moja  duniani na mbinguni kwa hiyo ndugu msomaji wa kitabu hiki ambacho hakikuwahi kutungwa na mtu yeyote zaidi yangu mimi mtunzi.Natoa ujumbe kwamba utajiri wote ni wa Mungu bila MUNGU kuamua Matajiri hao wasinge pata huo utajiri

Mfano mzuri Katavi kuna mtu alikuwa anachimba choo akakuta dhahabu na akawa tajiri  hayo ni mapenzi na mipango ya MUNGU bila ya yeye hakuna linaloshindikana  kila kitu unachokiona duniani ni mali ya MUNGU na MUNGU kupitia uwezo aliokuwanao  ndiyo anawafanya watu kuwa matajairi.

Hakika Kila kitu unachokiona ni mali ya MUNGU sababu kimetoka ardhini   dunia bila MUNGU ingekuwa kama jangwa  nahii  inapelekea  kuamini kuwa MUNGU yupo.  Hata kwenye kitabu nilichokitunga  cha maajabu ya MUNGU katika uumbaji wa dunia nimeleza kinagaubaga jinsi MUNGU alivyoweza kuumba mbingu na dunia na vitu vyote vinavyoonekana na visivyoonekana kwa macho moja kwa moja kwamba kimeumbwa na Mwenyezii MUNGU kitabu hicho kinapatikana.

 

Mahitaji makuu ya binadamu  NIAOROZESHA KIFUPI UTAJIRI KATIKA MALAZI

Nilishaeleza bayana kuwa tajiri anayetambulika katika malazi ni yule anayemiliki nyumba kali na gari kali ambavyo wengi hawana  kati ya watu yeye anamiliki gari la kwanza duniani na nyumba zote.

UTAJIRI KATIKA MAVAZI

Tajiri anavaa mavazi ya gharama sana mavazi ya tajiri gharama yake sawa na bajeti ya mtumishi wa serikali kwanza ameajiriwa mpaka anakuja kustafu maana yake mawazo yake yana dhahabu  jiulize hizodhahabu zimetoka wapi?  Maana  yake zimetoka ardhini zimeumbwa na MUNGU.

UTAJIRI KATIAKA CHAKULA

Tajiri anaongoza kula vizuri kuliko mtu yoyote duniani japo japo kuwa chaajabu zaidi unaweza kupewa chakula cha kutosha lakini ikakaosa apetite ya kula na hauwezi  kunununua kokote hali aliyoumba MUNGU.

Tumeongelea utajiri katika mavazi ,chakula na mavazi chakujiuliza ni kwamba vitu vyote vimetoka wapi?Bali jibu lake vimetoka kwa MUNGU. Hii inamaana bila nguvu za Mwenyezii MUNGU  na ndio maana kitabu tulichotunga kwa MUNGU wote tupo sawa nimeeleza bayana kwamba mbinguni hakuna masikini wala tajiri wala hakuna wanaokula chakula kizuri  au kibaya hakuna mtu ambaye ana gari na asiye na gari mbinguni watu watu wote ni sawa lakini kwa elimu ya duniani  watu hatuko sawa kama tajiri mtoto anaweza kusalimiwa na kupewa kiti lakini tofauti na mtu mzima  masikini mfano nimeshuhudia mimi mwenyewe  mtu mzima anasalimia mtoto kwa sababu ya fedha alizonazo mtoto na maana kinacho salimiwa ni utajiri wake unampa heshima lakini yote hayo huishia tu kwa tajiri wa matajiri ni Mwenyezii MUNGU yeye ndio mwasisi yaani mwanzilishi. 

 

 

 

Maoni

Machapisho Maarufu