TUISHI MAISHA YA UTAKATIFU

 

SURA YA PILI

KUMWONA MUNGU NI KAZI.

Ni ukweli usiopingika kuwa Wakristo ni wengi sana  lakini wanaoishi ukristo ni wachache sana. Na ndio maana hata kwa sisi wakiristo wakatoliki wanaotangazwa kuwa ni wenye heri ni asilimia moja tu Hii ni kutokana na ukweli usiopingika kuwa binadamu ni wengi sana ila wenye ubinadamu ni wachache.

Baada ya tafakari hiyo ndio kupitia uwezo wa Mungu ukaniongoza niandike kitabu kipya kuonesha kwamba Kumuoona Mungu(Utakatifu) Ni kazi, jinyime ya dunia uone ufalme wa mbinguni.

Roho mtakatifu aliniingia ilikuwa ni tarehe  30/11/2025 ambao ndiyo mwisho wa mwezi wa kumi na moja (11). Ilivyofika asubuhi majira ya saa kumi na mbili , Mwenyezi Mungu alinisihi niende kusali misa zile za asubuhi sana ambazo ni misa za majitoleo maana unakuwa umejinya usingizi mtamu ule wa saa kumi na mbili. Na ilikuwa hivi, nimeamka saa kumi na mbili asubuhi. Katika ya usingizi mzuri na mkali sana  ghafla sauti ikaja. James  Amka, embu  hesabu moja hadi ishirini. Nikahesabu moja hadi ishirini nikawa nimeamka kwenda kusali misa ya asubuhi.

Siku hiyo ya tarehe 30.11.2025 ndio chem. Chem. Ya kitabu change hiki ambacho ukikisoma vyama na kuishi zile her inane basi automatic lazima uende mbinguni.

Pamoja na mambo mengine siku hiyo hiyo ndio iliumba msingi wa kitabu hiki kizuri kuwa kumbe kumuona Mungu( utakatifu) Ni kazi. Sio kwa sababu niliamka asubuhi na kenda kanisani , hapana, kwenda kusali kanisani ni jambo jingine na utakatifu ni jambo jingine. Mbona nimeeona watu wengi wakiamka saa kumi na mbili kwenda kusali kanisani ila akirudi kauli zake ni kaa mtu tu ambaye hajaenda kanisani. Maana kuna baadhi wanaenda kanisani kwa mazoea tu na wengine wanaenda kanisani kujionesha ila kwenye kuuishi ukiristo unakuta hauishi ukiristo kama anavyotakiwa kuishi maana ndani yake anakuwa na roho ya matusi, majibizano, kiburi na kujikweza tofauti na mafundisho na Makatazo mbali mbali katika bibilia.

 

Msomaji wa kitabu changu , chochote kile kinachoufurahisha mwili  kama vile usingizi mtamu,  au roho ya uvivu inatakiwa upingane nayo. Nenda ukasali asubuhi ili kujitoa sadaka huku ukiacha watu wengine wakifurahia usingizi wa asubuhi. Popote ulipo kama utatumia pikipiki kama utatumia usafiri gani, lakini kujinyima kwa ajili ya kwenda kanisani kutekeleza majukumu ya kusalii ni heri kubwa sana na ni hazina kubwa sana

Watu wengi wanapata baraka pasipo kujijua hizo Baraka wanapataje pataje kumbe jibu lipo wazi ni  kwa sababu wanasali kwa kujitoa  . Kwa hiyo, tujitoe miili yetu kwa Bwana kwa   kuamka asubuhi kwenda kusali huku akiacha wengine wakiwa wanakoroma, wakiwa  wanafurahia ile raha ya usingizi kwani usingizi ni raha.

Mifano hai tunayo, ipo ivi, mtu alikata tiketi yake kwa ajiri ya kusafiri alufajiri huwa anashikwa na usingizi mzito sana. Huo ni usingizi wa saa kumi na mbili   . Hali hiyo pia ni sawa na mtu anayejitolea kuamka alfajiri kwa ajiri ya Kristo na kwenda kusali kanisani.

Hii inaonyesha kwamba kulala ni style nzuri sana ambayo inamfanya mwanadamu afurahie maana kuna  raha furani ambayo mwanadamu huipata kupitia usingizi.

Sasa unapokuwa unaenda kanisani kusali asubuhi maana yake unajitoa sadaka au ni mafungo fulani ambayo Mungu anayapokea kama sehemu ya majitoleo yako na  inakufanya wewe upate baraka fulani ambazo wengine hawazipati.  Baraka unazozipata ni pamoja na tiketi ya  kumwona Mungu.Lakini tiketi hii ili ikamilke inatakiwa pia uwe unaziishi na zile her inane pamoja na kutii amriza Mungu na amri za Kanisa.

Hivyo kitabu hiki kitakufaa wewe mkiristo kwa kukusaidia kwenda kusali asubuhi na ikane roho ya uvivu inayokutaka uendelee kulala.

Kitabu hiki kitamsaidia hata mtunzi wa kitabu kuanza kusali asubuhi kwa ajili ya kupata baraka na neema. Ili na mimi nisiwe kama wapiga debe stendi wanaosema ingieni kwenye gari msafiri alafu wao hawasafiri. Katika maombi yangu, nimemuomba Mungu anisaidie kamwe nisiwe kama wapiga debe kwenye gari wanaopiga debe kwamba ingieni kwenye mabasi , basi likanza  kudondoka wapiga bede wanabaki.  Hii ina manana kuwa kitabu hiki kinisaidie hata mimi mwenyewe kumuoona Mungu kwa kujitesa duniani na kujima.

 

Angalia kava ya kitabu hiki ambacho nimechora mtu mkubwa wenye matawi mengi

 

 Waumini Wanaofurahia usingizi wa asubuhi ni wengi sana ila wanaoenda kusali  kanisani  ni wachache sana. Katika wakiristo mia utapata ni mkiristo mmoja tu anaye amka na kwenda kusali asubuhi.  Ni ajabu sana ukiangalia wakiristo wakatolki ni wengi sana  lakini wanaojitokeza kwenda  wachache sana. Kwa hiyo tuitumie miili yetu kuitesa kwa  kuamka asubuhi ili mwisho wa siku sadaka hii Mungu ataitumia. Kukupa wewe thawabu. Kukusaidia wewe kukukinga na mambo mabaya pasipo wewe binafsi kujijuwa  

 

Msomaji wa kitabu change ninakusihi uweze kuutesa mwili wako kwa kudamka sana asubuhi na hatimaye kwenda kusali kwa dhati kabisa huku ukiacha baadhi ya binadamu wakiwa wamelala sisi Wakatoliki tuko wengi sana mamilioni ya mamilioni ya Wakatoliki na duniani tupo hadi bilioni na ushee   lakini wakatoliki watakaomuoona Mungu ni wachahche sana. Nakuomba msomaji wa kitabu hiki vumilia shida za dunia, ipo siku utamwona Mungu utafarijika.

Duniani hakuna raha yoyote ile kwani duniani kuna mateso na dhiki za kila aina  hata namna ya kuelezea shida za dunia nina shindwa.

Yani duniani uishi kwa shida nyingi alafu ukifa ukachomwe motoni.

Kwa hiyo, nakuomba wewe msomaji wa kitabu changu muumini mwenzangu jitese kwa  kuamka asubuhi kwenda kusali, kitanda na mwili havinaga  shukrani. Hata ulale vipi  mpaka saa sita mchana au  saa saba,  utaamka tu na usingizi utaisha na utapotea utasahau kana kwamba haukulala

 

 

 

 

Maoni

Machapisho Maarufu