TUKISEMA HATUNA DHAMBI TUNAJIDANGANYA

 


SURA YA PILI

TUKISEMA HATUNA DHAMBI TUNAJIDANGANYA

Kilichonichechemsha mpaka kuandika sura ya pili ya kitabu hiki, inayosema, “TUKISEMA HATUNA DHAMBI TUNAJIDANGANYA”.  Ni baada ya kusoma Biblia vizuri sana kinagaubaga na kugundua kwamba kuna mistari katika Biblia inayoeleza bayana kwamba wanadamu tumejawa na dhambi, na kwamba tukisema hatuna dhambi tunajidanganya wenyewe, na kwamba binadamu tumezaliwa tukiwa na dhambi ya asili isipokuwa tu, Mama Bikira Maria mkingiwa dhambi ya asili. Madhumuni ya kuwatungia watu mbali mbali kitabu hiki  ni kuendelea kuelimisha wasomaji wa kitabu hiki kwamba sisi binadamu ni wadhambi, na hivyo ili tuweze kupata uzima wa milele, inabidi dhambi zetu tuweze kutubu. Kwa hiyo, kitabu hiki ni meli ya kukuvusha juu ya maji ili usizame bali ukamuone Mungu. Kwa tafsiri nyepsi kitabu hiki kinakusaidia wewe kumuona Mungu kwa kutubu dhambi zako. Hapo inakuwa ni kama tiketi ya moja kwa moja kutoka duniani kwenda Mbinguni.  

Pia kitabu hiki kimeeleza kinagaubaga kuwa moja ya  Sakramenti za Wakatoliki ni sakramenti ya kupata Komunio. Tunampokea Yesu kupitia umbo la mkate na divai.  Hiyo ni Imani kali ya kanisa katoliki . Yesu Kristo anakuwa yuko ndani ya moyo wako. Na Yesu Kristo ili aweze kuwa ndani ya moyo wako inatakiwa moyo wako wewe uwe na moyo ambao ni moyo msafi. Yesu Kristo hapendi nyumba ambayo siyo safi, nyumba ambayo ina wageni wengi na hapo ni pale unapo karibisha vitu vingi ndani ya moyo wako, kunakuwa na chembechembe za wizi ndani ya moyo wako.

Chembe  chembe za ushirikina, na chembe za uchawi ndani ya moyo wako. Ndani ya moyo wako kunakuwa na kiburi na dharau ya kutokumtii, mke au mume ndani ya moyo wako unakuwa na wapangaji wengi. Yesu anataka nyumba iwe haina mpangaji yoyote yule. Hivyo mwandishi wa kitabu hiki anakushauri wewe msomaji wa kitabu uondoe wapangaji wote  na baki Yesu peke yake. Njia pekee ni kufukuza wapangaji kupitia kutubu dhambi zako na unatakiwa kuungama kwa padre.

 

 

 

 

Maoni

Machapisho Maarufu