TUSIANGALIE PICHA ZA EX KWENYE MITANDAO
SURA
YA TATU
KUMWONA
MUNGU NI KAZI.
TUSIANGALIE
PICHA ZA UTUPU KWENYE MTANDAO
Kwa
Wakristo wenzangu Wakatoliki, kamwe tusiendekeze
kuangalia picha ambazo hazimpendezi Mwenyezi Mungu. Wapo baadhi ya wakiristo wenzangu wananunua Mb na bando la
kutosha kwa ajiri ya kuangalia picha za
utupu. Mungu hapendi kabisa kumuoona muumini wa kanisa katoliki akiangalia picha
za utupu.
Huwezi kabisa kupata Baraka za mwenyezi Mungu.
Wapo baadhi wanadiriki kabisa hadi kukopa pesa ili anunue bandle angalie picha
za utupu za wadada wanao danga ambao wanafanya
kazi za umalaya. Hiyo ni dhambi kubwa sana. Unapoangalia picha za utupu katika
mitandao ya kijamii inamaana unakuwa umekengeuka kweli kwani Mungu hawezi kukubariki kwani na wewe
pia unakuwa umekuwa mshirika au muumini wa vitendo ambavyo havimpendezi Mungu.
Hivyo
huruhusiwa kabisa hata kukomonika maana Yesu hawezi kukaa nyumba moja na
shetani kwani tayari kwenye nyumba yako kuna posti ambayo machapisho hayampendezi Mwenyezi Mungu kwani ni ibada ya
kumtukuza shetani.
Machapisho
yanayoenda kinyume na imani za sisi Wakristo Wakatoliki kwani yana kinzana na
usafi wa roho. Post za video kwenye
mitandao ya kijamii zinaonesha picha za wanawake walio uchi ni post zinazomdhalilisha mwanamke na zinaonesha picha
za uzinifu picha zinazo hamasisha uzinzi.
Hiyo
ni dhambi kama zambi nyingine. Mkiristo mwenzangu! Usijiingize kwenye dhambi
isiyo ya lazima kwani unakosa nini? Badala ya kupokea baraka kutoka kwa
Mwenyezi sasa unapokea mikosi.
Kama
una rafiki ambaye ana weka kwenye profile yake picha za uchi au za kuonesha
utupu wa mwanamke basi rafiki huyo ni bora uweze ku –block. Posti
za video katika mitandao ya kijamii zina
mkufuru Mungu na kumfundisha Mungu kwamba aliumba kwa kukosea. Mungu amemtumia
wakili James Lubus kukufikishia ujumbe kuwa ukitaka kumuoona Mungu lazima
uepukane na tabia ya kuangalia picha za utupu mtandaoni
Na kama una hizo link unatakiwa kuzi -block
ili usije ikazioona tena. Tambua kwamba kwa sisi wakiristo katika vitu ambavyo Mungu hapendezwi navyo ni
pamoja na ibada za kumwabudu Shetani. Hii
ni ibada za kuangalia picha za
uchi mitandaoni hasa hasa wakinamama wakiwa wapo uchi. Pamoja na picha za wadada wanao danga danga mitandaoni.
Na
wewe dada Muombe Mungu akupe mchumba wako sio unatafuta wachumba mitandaooni
kwa kupost picha yako, Mungu hapendi.
Waswahili
wanasema, ‘Ndege wa kundi moja huwa wanaruka pamoja.’ Hivyo kama wewe sio mfuasi
wa Mungu basi lazima utakuwa mfuasi tu wa shetani maana wanaofanya hayo mambo ya kupost picha za uchi mtandaooni ni watu wa shetani. Mkiristo mkatoriki ninakuoomba usikubali kamwe kukosa tiketi ya
kumwona Mungu kwa kuangalia vitu ambavyo havimpendezi Mwenyezi Mungu
Tafuta
nyimbo za kikatoliki uweze kuzifuatilia na kuzifatisha kuziimba. Tafuta Video
nzuri za kikatoliki za kusifu na kuabudu zipo mtandaoni. Hapo ndio utakuwa
unatafuta tiketi ya kumuuona Mungu.
Hivyo
mpendwa sana msomaji wa kitabu changu, ninakuibia siri kubwa kwamba ukitaka
kabisa kumuoona Mungu nina kusihi kabisa
kama una tabia ya kuweka bando kwa ajiri ya kunagalia picha za utupu na
machapisho ambayo hayampendezi Mungu basi utakuwa unartafuta tiketi ya kuingia
Motoni na sio ya kumuoona Mungu.
Kama
una tabia hiyo unaweza ukaanza kuicha leo baada ya kusoma kitabu hiki na kama
huwezi kuacha tabia hiyo basi Muombe Mungu kwa Imani kubwa atakusaidia kwani kuendelea picha za utupu mtandaooni unakuwa
unaokosa Ufalme wa Mbinguni badala yake unakuwa unatafuta tiketi ya kwenda kwa Shetani.
Katika
moja ya vitabu vyangu nilivyotunga nimeeleza kwamba Mbinguni kuna raha kubwa
sana kuliko tafrija, sherehe, hafla, shangwe yoyote ile ya hapa duniani kwani
Kuna
viumbe wanaomsifu na kumwabudu Mungu na ndio maana kwenye kitabu changu hiki
nimeeleza kwamba Kumuoona Mungu ni kazi maana
sio wote walioteuliwa kushuhudia Mungu akisifiwa na Malaika na Watakatifu
Mbinguni ambao hutumia vifaa mbalimbali
vya kumsifu , kumtukuza Mungu , kama vile kengele, kinubi, vinanda. Na wanapiga
piga vitu mbalimbali vinavyotoa sauti nzuri inayompendeza Mwenyezi Mungu huku
wakiinua macho yao juu na wengine wakiwa wamelala kifudi fudi huku wakiwa
wanamsifu Mungu aliye waumba na Mungu
wakiwa wamemweka katikati na huku akiwa amezungukwa na viumbe vya ajabu ambavyo
vimeumbwa na Mungu mwenyewe na viumbe vingine vinachezea vinanda katika hali
inayoleta furaha isiyo na kifani mbele ya kiti furani cha ajabu ambacho
hakielezeki na kukiona tu unapata raha ya ajabu. Huku wengine wakiwa
wanamzunguka Mungu wakifurahi tu kumuoona na wengine wakiwa wanashuhudia jinsi
Mungu akiwa anasifiwa.

Maoni
Chapisha Maoni
thank you very much asante sana