TUSIUNGAME DHAMBI ZETU KWA AJILI YA KUKOMONIKA
SURA YA TANO.
TUSIUNGAME DHAMBI
ZETU KWA AJILI YA KUKOMONIKA
Nimetumwa
na mwenyezi Mungu nifikishe ujumbe jinsi ulivyo.
Kuna
baadhi ya watu huwa wanaungama kwa ajili ya kwenda kupokea sakramenti tu baada
ya kupokea sakramenti anarudia tena dhambi zake zile zile . Maana ya kuungama.
Kusikitika kwa dhambi ambazo amezifanya na pia kutamka kwamba hutafanya dhambi
tena. Hivyo kabla ya kuungama maana nyingine zaidi ya kufanya kwa ajili ya
kwamba tu uende kukomunika. Watu wakuone na waseme na leo furani amepokea
Ekaristi takatifu. Lengo la kuungama ni kwa ajili ya kujuta dhambi zako na
kukiri kwamba uliyoyafanya siyo sahihi mbele ya macho ya Mwenyezi Mungu, na
baada ya hapo unapokea sakramenti. Hapo hata kama ukibahatika ukafa siku hiyo
hiyo baada ya kuungama na kupokea sakarament takatifu unaweza ukamuoona Mungu
siku hiyo hiyo. Hivyo muombe Mungu akujalie kifo chema ambach ni kifo baada ya
kuungamana kupokea Ekarist Takatifu na wewe unaweza ukamuoona Mwenyezi Mungu na
sio lazima mpaka utangazwe mwenye Heri.
Kuna baadhi ya watu wametutangulia mbele ya macho ya dunia ila tunaamini ni
wenye Heri. Yupo padre mmoja anaitwa Padri Luka. Matendo yake yanatuonesha
kabisa ni mwenye heri na huko alipo
amuombee mwandishi wa kitabu ili Mungu apokee maombi yake kumi ambayo
alisali katika mlima mwana Uholo pamoja
na barua yake aliyomwandikia Mungu ya tarehe 14.10.2025 katika mlima wa
Itwelel.
Pokea
sakramenti kwa mujibu wa sheria za Kikatoliki. Pale ambapo ulidhamiria kuungama
kwa ajili ya kujionesha kwa watu ili upokee sakramenti na watu wote wakuone
kama ulipokea sakramenti. Unafuata taratibu za Kikatoliki lakini moyoni mwako
ulifanya hivyo kwa ajili ya lengo la kupokea tu baada ya kuungama na unaendelea na matendo yako yale yale. Huu sio
Ukristo. Maana kamili ya kuungama ni
kukubali kwamba umetenda kosa na hutarudia kosa. Kwa hiyo msomaji wa kitabu
changu usije ukaungama halafu unarudia
makosa yale yale ni dhambi kubwa sana. Biblia imesema kwamba tukisema hatuna dhambi,
twajidanganya wenyewe. Lakini tuchukulie kwamba Mungu aliweka. Mwadamu
anapozaliwa na dhambi ya asili, basi ndio muda wote kufanya makosa kwa Mwenyezi
Mungu.
Wapo
baadhi ya waumini kila siku dhambi ni
ile ile mpaka padre anamuambia umekuja kuungama zambi ile ile. Kuna baadhi huwa
wanabadirisha mapadri na kwenda kwa
mapadri wapya wengine ili wasisikie dhambi ile ile.
MUNGU
AKUBARIKI SANA
15.12.2025
.jpg)

Maoni
Chapisha Maoni
thank you very much asante sana