TUUNGAME DHAMBI ZETU

 


SURA YA TATU 

TUTUBU DHAMBI ZETU.

Katika sura hii ya tatu, nimeeleza kinagaubaga nini maana ya toba? Ni kujuta kwa kitu ambacho mtu amekifanya ambacho kwa fikira za kibinadamu inaonekana si kitu sahihi mbele ya macho ya Mwenyezi Mungu. Hii itakusaidia sana wewe msomaji wa kitabu hiki ambacho nimetunga mimi mwenyewe pasipo kukopea sehemu yoyote ile kupitia msaada wa kipaji cha Mwenyezi Mungu.

Kwa hiyo kitabu hiki kitakusaidia wewe kutubu dhambi zako. Ina maana kitakusaidia wewe moja kwa moja kwenda kuungama dhambi zako kwa Padre na baada ya kuungama dhambi zako zote ulizozitenda na dhambi ambazo nyingine ambazo umeisahau. Sisi binadamu tumekuwa ni wadhambi sana. Wakati fulani unatenda dhambi nyingine mpaka unakuwa umeisahau na kutubu dhambi zetu na kubariki na kukusamehe dhambi kwa niaba ya Yesu Kristo.

Nimeeleza bayana kwamba Biblia yenyewe imeeleza bayana kwamba yatakayoweza kufunguliwa duniani na mbinguni yatafunguliwa. Duniani na mbinguni pia yatafunguliwa kinagaubaga tena sana kwamba Mamlaka ya Hifadhi kukusamehe dhambi. Hayakuanza leo. Yalianza kipindi kile cha Yesu Kristo mwenyewe kabla ya kupaa mbinguni, aliweza kumteua Kuhani Mkuu ambaye ni Petro ili aweze kuwa na mamlaka yote juu ya Wakristo wote wa Katoliki. Na sasa hivi ndio Baba Mtakatifu ambaye kwa sasa yuko hapa na yeye.

 Sasa hivi Baba Mtakatifu amevaa viatu vya Petro. Hivyo hivyo viatu hivyo amempatia Padri ambaye sasa anakuondolea Dhambi .

Sasa  Mungu atakapo kuwa amekusamehe dhambi zako zote kupitia padre na Mungu pia anaweza kukusamehe dhambi zako zote. Baba Mtakatifu ametoa mamlaka hiyo kwa Makadinari na Maaskofu na wao wametoa mamlaka hiyo kwa mapadri.  

Ikumbukwe kwamba Baba Mtakatifu pia naye ni padri. Askofu ni Padri, hata Kadinari pia ni Padri.  Majukumu hayo yote waliweza kupewa kipindi kile ambacho Yesu Kristo mwenyewe kabla ya kupaa mbinguni aliweza kutoa madaraka hayo kwa mapadri mbalimbali ambapo aliweza kuwapa madaraka mapadri kuweza kuwaondolea watu dhambi zao.

Pindi tu pale watu wanapokuwa wanaona wamekosea na wanatakiwa waweze kuungama dhambi zao. Hivyo msomaji wa kitabu changu. Tukiri kinagaubaga kabisa moyoni kuwa tumefanya dhambi. Yote uliyoyafanya hayakumpendeza Mwenyezi Mungu na hivyo Mungu kwa huruma zake aweze kukusamehe  dhambi zako zote na kukusamehe. Kupitia padri tayari dhambi zako na kwao umeondolewa. Na hapo teyari ukimpokea Yesu Kristo. Kupitia. Mwili. Na damu ambayo ni mkate na divai. Yesu anaingia moyoni mwako akikuta moyo uko safi kabisa. Ni kama vile nyumba umeisha Safisha. Na sabuni na marashi yaani usanifu ipasavyo.

Yesu Kristo anakuja moyoni akiwa na sherehe na shangwe safi sana. Anajua yuko peke yake na utubu dhambi zako. Kitendo cha kukusamehe dhambi zako tayari na Mungu naye anakuwa amekusamehe. Umedhamiria kwamba na kuwa padri kuungama dhambi kwamba yale ambayo uliyafanya sio sahihi kwenye macho ya Mwenyezi Mungu na hivyo atakusamehe dhambi zako. Baada ya kutubu. Dhambi zako, padri atakubariki na atakusamehe dhambi zako na pia atakupa malipizi. Maana yake ni kwamba Mungu sasa atakusamehe na atakupa malipizi kwa kusali sala mbalimbali. Kusali Rozari. Kutubu kusali baba yetu marangapi. Ni tofauti na sheria za nchi mfano  angalia, umefanya kosa kubwa kama vile umeua au umevunja na kuiba. Serikali itaamuru na wewe unyongwe hadi ufe au ufungwe.  Kwa sheria za nchi yetu ukifanya kosa,  adhabu yake ni kwenda gerezani utajutia. Lakini Mungu alivyokuwa na huruma ukifanya kosa lako anachokifanya yeye ni kukusamehe tu kukupa malipizi tu. Yaani hata dakika tano hazifiki.

Baada ya kusali sala ya salamu Maria mara kadhaa  na sala mbalimbali ambazo padre atasema unatakiwa uzisali, ukipiga hesabu  ya muda hata dakika tano hazifiki. Hata  kama umeua, ukienda kwa padri ukisema  niliua  padre hawezi kukukamata na kukupeleka polisi au mahakamani. Atakusamehe dhambi zako na atakupa malipizi ya kwamba nenda ukisali Salamu Maria mara tano na Mungu pia  anakuwa amekusamehe na unapotubu. Maana yake umekubali kwamba wewe ni mdhambi. Na Mungu aweze kukusamehe dhambi zako.

Maoni

Machapisho Maarufu