Ruka hadi kwenye maudhui makuu
UNGAMA KWANZA NDIO UPOKEE

Mpendwa msomaji na mfuatiliaji wa kitabu
changu ambacho nimetunga mimi mwenyewe. Kila sehemu kuna taratibu zake. Kwa
sisi Wakiristo Wakatoliki ambapo mimi ni
mmoja wapo. Ni agizo kwamba kabla ya kuungama na kupokea sakramenti ya komoniao
unatakiwa kuungama dhambi zako kwanza kwa makosa ambayo umeyafanya baada ya kujuta
dhambi zako. Sura ya tatu nimeeleza kwamba
tayari Mungu anakuwa amekusamehe
dhambi zako na sasa moyo wako unakuwa safi kwa ajili ya kumruhusu mgeni aweze
kuingia moyoni mwako. Mgeni huyu ni Yesu Kristo ambapo sasa anaingia moyoni
mwako kwa kugonga hodi na sasa na wewe sasa kumkaribisha moyoni mwako anakuwa
ni mgeni wako.
Kwa
wakiristo Wakatoliki ni agizo la miaka nenda rudi karne kwa karne. Kwamba kabla
ya kupokea Sakramenti takatifu inatakiwa utubu dhambi zako zote ambazo
amezifanya. Angalizo endapo utapokea sakramenti kabla ya kuungama ina maana
wewe unakuwa umeenda kinyume na maandiko ya Kanisa Katoliki ambayo inatokana na
sheria ya Kanoni, ambayo imeeleza bayana kinagaubaga kwamba Mkristo yeyote yule
amesamehewa dhambi zake mara tu baada ya kuungama. Tayari. Moyo wake unakuwa ni
moyo safi na hapo anakuwa tayari kwa ajili ya kupokea Sakramenti Takatifu.
Endapo umepokea sakarament kabla ya kuungama dhambi ina maana unakuwa unakula
hukumu yako mwenyewe. Upo wimbo ambao huwa unaimbwa wakati watu wanaendelea
kukomunika? Unasema kwamba anayekula mwili wangu bila kuungama anakula hukumu
yake mwenyewe. Anayekula mwili wa Kristo kabla ya kuungama. Ina maana yeye
binafsi anakuwa anafurahisha tu wale watu ambao wanamuona. Upande wa Mbinguni anakuwa anapokea na kula ukoko wa ugali
anakuwa sio Yesu Kristo. Mwili kamili wa Yesu Kristo unageuka kuwa hukumu yake
yeye mwenyewe binafsi anapoenda kuupokea mwili wake.
Taratibu
za kidini ambazo zimewekwa na Kanisa Katoliki zimeelezwa kwamba mtu asiye
mpokeA Yesu anakosa mambo mengi sana ikiwa pamoja na vibaraka vilivyotokana na
Sakramenti Takatifu ya Komunio. Kwa hiyo anayeweza kupokea Ekaristi Takatifu
bila kuungama anakuwa anafanya kosa mbele ya Mwenyezi Mungu kwani anakuwa
anawafurahisha tu watu ili watu waweze
kumwona kama ni mkristo mzuri ambaye anatekeleza taratibu za kupokea sakramenti
kama zilivyo kwenye dini . Hata wenzetu waislamu wana nguzo za Kiislamu
Hata
sisi wakiristo wakatoliki tuna nguzo
ambazo ni Skrament mbali mbali na moja ya Sakrament hizo ni kitubio na
Komunio ya kwanza. Ni Sakramenti Takatifu ambazo mtu anazipata baada ya
kuungama dhambi zake zote na kusamehewa na Mwenyezi Mungu. Mungu sasa moyo wake
unakuwa ni Moyo Mtakatifu tayari kwa ajili ya kumpokea mgeni kama nilivyoeleza
katika Chapter ambazo zimepita msomaji wa kitabu changu. Cha kuomba kwamba.
Najua ungama dhambi usipokee. Kuna baadhi ya wakiristo wenzangu wanajidanganya bure.
Wanasema kwamba hamna haja ya kuungama kwa
padre bali unatakiwa kusali sala ya majuto ambayo ni
‘’Mungu wangu najuta dhambi zangu zote, kwasababu nimekukosea na
kukukasirisha wewe, muumba wangu Mwenyezi, Baba yangu na mkombozi mwema,
usinitupe wala usinikatae, nataka kuacha dhambi na nafasi zangu zote
zinazonifanya nitende dhambi, ili nishike maagano haya, AMINA.”
Au sala ya Nakuungamia
Nakuungamia
Mungu Mwenyezi; nanyi ndugu zangu, kwani nimekosa mno kwa mawazo, kwa maneno,
kwa vitendo na kwa kutotimiza wajibu. Nimekosa mimi, nimekosa mimi, nimekosa
sana. Ndio maana nakuomba Maria mwenye heri, Bikira daima, Malaika na
watakatifu wote, nanyi ndugu zangu, niombeeni kwa Bwana Mungu wetu.
Mungu Mwenyezi atuhurumie, atusamehe dhambi
zetu, atufikishe kwenye uzima wa milele. Amina
Sio njia mbadala ya sacrament ya kitubio. Sala
hizo unaweza ukazitumia kama huduma ya Mungamo haipo au padre hayupo jirani na
una hatari ya kufa bila kutubu.
Tujiulize
kama kulikuwa na sala hizo kulikikuwa na maana gani ya sacrament ya kitubio?
Sala ya majuto, nakuungamia na sala ya Bwana utuhumie sio mbadala wa sacrament ya kutubu.
Hizo ni sala za kawaida ambazo wakati uko
mbali na padri, unaweza kusali sala na Mungu kwa huruma yake akusamehe. Siku
hizi baadhi ya Mapadri wamekaa tu bila kuwa na kazi ya kuwaungamisha watu maana
padre hawezi kukufuata nyumbani kwako akuite uende ukaungame dhambi zako. Yani
dhambi utetnde mwenyewe alafu padre akufuate nyumbani kwwako. Labda uwe unaumwa
tu.
Kwa
kuhitimisha, topiki hii nimetumwa kutoa ujumbe kwamba tusipokee sakramenti kabla ya kuungama. Mjumbe
hauuwawi. Isije mwisho wa siku ukasema Wakili hakukufikishia ujumbe.
Maoni
Chapisha Maoni
thank you very much asante sana