UTAKATIFU (KUMUNA) MUNGU NI KAZI


SURA YA TANO

UTAKATIFU NI PAMOJA NA KUACHA DHAMBI YA KUSEMA UONGO

Msomaji wa kitabu changu hiki ambacho kama ukifuata haya ninayokueleza, hakika utapata tiketi ya kumwona Mungu

 Katika dhambi ambazo zinawatesa mno  binadamu ni pamoja na dhambi ya kusema uongo ambayo ni dhambi inayotesa wakiristo wengi kwa sababu dhambi ya uongo imekaa katika sehemu tatu ambazo ni kiuchumi, kisiasan akiutamaduni.  Kupitia uongo, mtu anaweza akajipatia kipato ambacho sasa kinaweza kuisaidia familya yake na mapato mengi ya shuguli binafsi za binadamu yanatokana na kusema uongo. Dili zote za mitaani zinapatikana kupitia kuvunja amri ya Mwenyezi Mungu ambayo imesema usisieme Uongo maana watu wengi wanajipatia riziki kupitia uongo.

Hivyo ungo unampatia mtu chochote kitu. . Mtu Anaweza pia akimdhihaki Mungu kupitia uongo kwa kujifanya anasali sana.

Hivyo ili kumuoona Mungu mimi na wewe inatakiwa tujiadhali na dhambi ya Uongo. Hivyo msomaji wa kitabu change hiki ninaomba tusiseme uongo ili tuweze kukuooona Mungu.  

Watu wengi huwa wana idharau sana hii amri ya Mungu ya kutokushuhudia uwongo na wanachukulia poa sana. Mungu sio mwanadamu alichokikataza lazima ukifuate

 

Kuna baadhi ya wasomaji watasema mbona huyu ni mwanasheria na wanasheria kusema uongo ndio mahali pake! Nani kakwambia.  Kupitia Roho Mtakatifu Mungu amenituma nitunge kitabu hiki   ili ujiepushe na dhambi ya uongo.

Hata wewe msomaji wa kitabu hiki pia uweze kujiepusha na dhambi ya uongo. Mungu aliweka amri zake ili ziweze kufuatwa na sio kupuuziwa.  Utakatifu ni kazi mno na hivyo ili uweze kuingia mbinguni inabidi uepukane kabisa na kusema uongo. Inabidi sasa uende kujifunza kusema ukweli.  Na ukweli wa dhati unamuweka mtu huru kabisa. Kuacha uongo ni kazi. Anza kwa kuacha uongo pale panapokutaka useme uongo sema ukweli kabisa na Mungu atakusaidia.  Kuna ukweli mwingine ukisema lazima ukose fedha. Ukisema ukweli pia lazima ukose utetezi. Kuna ukweli mwingine ukisema lazima ufukuzwe kazi. Kuna ukweli mwingine ukisema lazima ukuletee madhara mengi N akuna ukweli mwingine ukisema lazima ufungwe. Ila bora ufungwe na uje utoke kuliko kuuokosa ufalme wa mbinguni.

Kuna ukweli mwingine ukisema lazima ufungwe jela.. Hivyo taratibu kubaliana na madhara utakayoyapata. Mungu mwenyewe ndie atakae kulipa madhara hayo utakayokutana nayo.

Mimi na wewe sasa tumuombe  Mungu atusaidie kuepuka dhambi ya uongo ambayo itatufanya pia tusimuoone Mungu.  Kwa hiyo, msomaji wa kitabu hiki kizuri. Utakatifu ni kazi kubwa sana. Vumilia mateso yatapita tu kwa wakati yatakuwa ni mateso ya muda mfupi sana.  Na hivyo nakualika sasa uombe huruma ya Mwenyezi Mungu kwa kuungama   dhambi kwa padre. Na Padri atakusamehe makosa yako kwa kusema uongo ambao umefanya wewe ukapata mali nyingi. Uongo ambao umefanya wewe ukatoka kwenye hatua moja kwenda hatua nyingine. Lakini mwombe Mungu akupe riziki mbadala ya kusema uongo. Mungu mwenyewe alikuwa na maana yake kusema kwamba usiseme uongo.

Kama nilivyosema kwenye dhambi moja pia inatakiwa uzishike na kuzitii amri nyingine za Mungu

BARIKIWA SANA

Sasa Mwenyezi Mungu kazi zako za vitabu vitano ulivyoniagiza nimemaliza vitabu  vyako na sasa naomba unijibu maombi niliyoomba katika Mlima Itwelele pamoja na maombi kumi niliyoomba katika mlima mwana uholo. Asante sana. Vitabu vyenyewe ni

ü NAMPENDA MUNGU NITAUNGAMA  DHAMBI ZANGU NIPATE UZIMA WA MILELE

ü MUNGU ANASIFIWA NA MALAIKA NA WATAKATIFU WOTE MBINGUNI,  UNGAMA NAO KUPITIA SALA NA PAMBIO

ü KUMUONA MUNGU(UTAKATIFU) NI KAZI

ü TUMWABUDU NA TUMSIFU NA TUMSUJUDIE MUNGU

ü KWA MUNGU WOTE NI SAWA

ü MUNGU TAJIRI WA MATAJIRI

ü  

 

31.12.2025

 

LITANIA YA MTAKATIFU ​​PADRE PIO.*

*Bwana, utuhurumie.*

*Kristo, utuhurumie.*

*Bwana, utuhurumie.*

Kristo, utusikie.

*Kristo, kwa neema utisikie.*

Mungu Baba wa Mbinguni,

*utuhurumie.*

Mungu Mwana, Mkombozi wa dunia,

*utuhurumie.*

Roho Mtakatifu Mungu,

*utuhurumie.*

Utatu Mtakatifu, Mungu Mmoja,

*utuhurumie.*

Maria Mtakatifu, Bikira Safi, *utuombee.*

Mtakatifu Padre Pio wa Pietrelcina, *utuombee.*

Mpendwa wa Mungu, *utuombee.*

Mwigaji wa Yesu Kristo, *tuombee.*

Mchungaji mzuri wa watu, *utuombee.*

Mfano wa makuhani, *utuombee.*

Mwanga wa Kanisa, *utuombee.*

Mwenye kuabudu Sakramenti Takatifu, *utuombee.*

Mwana mwaminifu wa Mtakatifu Fransisko, *utuombee.*

Uliyetiwa alama na unyanyapaa wa Yesu, *utuombee.*

Mgonjwa katika mateso, *utuombee.*

Msaidizi wa wanaokufa, *utuombee.*

Mkurugenzi wa roho, *utuombee.*

Moyo wa dhahabu, *utuombee.*

Mtume wa rehema, *utuombee.*

Mtenda miujiza, *utuombee.*

Mfariji wa walioteswa, *utuombee.*

Mpenda Rozari Takatifu Zaidi, *utuombee.*

Msaidizi wa roho zilizo na mashaka na giza, *utuombee.*

Mfariji wa wagonjwa, *utuombee.*

Mfano wa unyenyekevu, *utuombee.*

Chanzo cha hekima, *utuombee.*

Kioo cha maisha ya kimungu, *utuombee.*

Mpenzi wa Yesu aliyesulubiwa, *utuombee.*

Umejiuzulu kwa mapenzi ya Mungu, *utuombee.*

Ulitenda mema duniani, *utuombee.*

Ulitejazwa na roho wa kujitolea, *utuombee.*

Msaada wetu na tumaini katika mahitaji yetu yote, *utuombee.*

Chombo cha Roho Mtakatifu, *utuombee.*

Unatuongoza kwa Kristo, *utuombee.*

Baba yetu wa kiroho na mtetezi, *Utuombee.*

Taji ya utukufu Mbinguni, *Utuombee.*

Mwanakondoo wa Mungu unaondo dhambi za dunia, *utuepushe, ee Bwana.*

Mwana Kondoo wa Mungu huondoaye dhambi za dunia, *kwa neema Utusikie Ee Bwana.*

Mwana Kondoo wa Mungu huondoaye dhambi za dunia, *Utuhurumie.*

*TUOMBE:*

*Mungu Baba yetu, Umemsaidia Mtakatifu Padre Pio kuonyesha sura ya Kristo kupitia maisha ya upendo na kujitolea.*

*Naomba tufuate Mwanao kwa kutembea katika nyayo za Mtakatifu Padre Pio wa Pietrelcina na kwa kuiga upendo wake wa kujitolea. Kwa njia ya Kristo Bwana Wetu.*

Maoni

Machapisho Maarufu