UTAKATIFU NI PAMOJA NA KUWASAMEHE WATU WALIOKUKOSEA

 

SURA YA NNE

UTAKATIFU NI KAZI PAMOJA NA

KUWASAMEHE  WALIOKUKOSEA

Hauwezi kwenda kanisani kusali bila kusali sala hii ambayo inaonesha kwamba kabla ya kwenda kanisani inatakiwa uwasamehe waliokukosea. Hayo sio maneno yangu na nakupeleka moja kwa moja kwenye bibilia,

MT 6;9-13

SALA YA BABA YETU

Baba yetu uliye mbinguni, jina lako litukuzwe. Ufalme wako ufike. Utakalo lifanyike duniani kama mbinguni.

Utupe leo mkate wetu wa kila siku. Utusamehe makosa yetu, kama tunavyowasamehe na sisi waliotukosea. Usitutie katika kishawishi, lakini utuopoe maovuni. Amina.

 

Nilikuwa nafanya mazungumzo na mwanandoa mmoja ambaye alishindwa kumsamehe mme wake lakini huku yeye alikuwa anasali  mara kwa mara. Kumbe maombi yake yalikuwa hayapokelewi kwa sababu alishindwa kumsamehe mme wake na pia alishindwa kujishusha mbele yam me wake. Baada ya kumwambia aweze kusamehe ndio Mungu akamfungua na akaanza kufanikiwa.

 

Moja kati kitu kinachowashinda watu wengi ni kitendo cha kusamehe na kusahau kabisa,yupo mtu anakwambia nimekusamehe ila sitaki mazoea au ukaribu na wewe tena,ndugu yangu huo si msamaha. Msamaha wa kweli ni ule unao toka moyoni na bado mnazidi kuwa na ukaribu na upendo pia.

Yupo mtu mwingine anasema nimesamehe ila akiongea na yule aliyemkosea hana raha kabisa anatamani amalize haraka kila mtu apite njia yake.  Hata akatokea amemuona yule aliyemkosea unaibuka uchungu usio wa kawaida ndani ya moyo wake,au kama amemuona anakuja njia hii basi yupo radhi kubadili njia asikutane nae bado nao si msamaha.

Mwingine anasema nimesamehe ila ikatokea yule ndugu aliyemkosea kapata matatizo fulani,unashangaa anafurahi ndani ya moyo wake ila nje anaonyesha kusikitika ndugu yule kupata matatizo nao huo tunasema hakuwa msamaha bali ni ulisamehe kinafiki adui yako akipata shida na ikiwa ulisamehe kwa moyo kabisa ikatokea kapata matatizo unapaswa kumuombea na ikiwa unaweza kumuona na kumtia moyo au kumsaidia katika matatizo yake unapaswa kufanya hivyo,Na hapo ndipo tunasema kweli ulisamehe.

 

Yesu anafundisha katika Mathayo 18:21-22 kwamba tunapaswa kusamehe “Sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini,” akionyesha kwamba msamaha si kitendo cha mara moja tu, bali ni mtazamo endelevu wa neema

 

Utakatifu pia ni  kazi ni pamoja na kusamehe watu waliokukosea. Moja ya vitu vigumu hapa duniani ni pamoja na kusamehe watu walioutesa moyo wako. Watu hao ni maadui zako ambao waliwahi kukutenda mpka ukaonekana sio mtu sahihi kabisa katika hii dunia.

 

Bibilia kupitia maandiko yake imeleza bayana kwamba inakupasa kuwasamehe wale wote waliokukosea. Kwa Mkristo Mkatoliki utake usitake ili kumuona Mungu ni lazima uwasamehe watu ambao walikosea.

Watu hao ambao walikupa wakati mgumu mpaka ukakufanya uwachukie hata ndugu zao na wote ambao wanandamana nao.  Watu hao huenda walikutakana mbeley aumati wa watu mpaka utu wako ukadhalilika ila Yesu Kristu anakutaka watu hao uwasamehe kabisa.

Nimeeleza kila kitu kuwa UTAKATIFU NI KAZI, moja ya kazi hii ngumu ni kukutaka wewe msomaji pamoja na mwandishi wa kitabu hiki kuwasamehe wale wote waliokutenda kwa namna moja au nyingine.

Na ndio maana njia ya kumuoona Mungu ni njia nyembamba kweli kweli maana duniani inakuwa ni njia ngumu sana ambayo watu wengine ambao hawawezi kusamehe watu walio wakosea hawawezi kuingia mbinguni.

Kusamehe ni kusamehe tu na haijalishi adui huyo amekukosea kiasi gani unachotakiwa ni wewe kusamehe waliokukosea na ukimaliza tu kusema nimekusamehe na Mungu naye automatiki anakuwa amekusamehe dhambi zako. Hivyo kabla ya kusamehe omba Mungu akusaidie uwe na moyo wa kusamehe.

Kuna watu wengine huwa wanasamehe juujuu tu huko sio kusamehe bali ni kusamehe kinafiki maana bado una duku duku moyoni mwako. Hapo unakuwa haujasamehe. Muombe Mungu akupe moyo wa kusamehe ili uwasamehe kweli kweli hao wote ambao wamekukosea. Mungu naye anakusamehe dhambi zako hapohapo.

 

Kumbuka kuwa wakiristo wote Baba yetu ilivyo kwamba utusamehe dhambi zetu kama sisi waliotukosea. Kupitia sala ya Baba yetu na kutaka wewe sali sala, uwasamehe wewe watu waliokukosea na kuwasamehe. Ni jambo la kujinyima kwamba ya duniani yatapita. Kwa hiyo. Msamaha uwe na amani ya moyo badala ya kusamehe pale moyo wako unakuwa na amani. Ni kweli unakosea sana. Hamtendei haki. Kuna wengine wanatumia mali zao kudhalilisha. Kwa kupitia kitabu hiki. Nitamke kwamba nimeamua kumsamehe. Kitabu hiki ni kutoka moyoni kweli kweli na ni kweli kupitia matusi. Siko karibu na hata wale watu ambao anafanya nao kazi kwa ukaribu. Mungu alinipa kitu fulani. Nikaona sasa hapa nitumie nafasi hii kuweza kusamehe na kusamehe kuona Ufalme wa Mbinguni. V. Neno kusamehe inatakiwa litoke ndani na nje. Neno hili linatoka ndani ya moyo wangu wote duniani. Lazima yatimizwe. Siwezi kubaki na kinyongo. Kuyachukia baadhi ya watu kwa sababu tu mtu mmoja anaweza kunitukana. Mungu aweze kunipa moyo wa ujasiri kama nisamehe na kusamehe kwelikweli. Na kusamehe maana yake ni kutamka kwamba nimemsamehe.

 

 

 

 

 

 

 

 

Maoni

Machapisho Maarufu